Joy FM

Waziri Aweso ataka mkandarasi kuongeza kasi mradi wa maji Kasulu

25 July 2025, 12:42

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso akiwa na viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Halmashauri ya Mji wa Kasulu mkoani Kigoma inakabiliwa na upungufu wa lita milioni 5 za maji kati ya lita milioni 15 zinazohitajika ili kuondoa changamoto ya uhaba wa maji safi na salama kwa wananchi.

Na Hagai Ruyagila

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso amemuagiza mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 uliopo halmashauri ya Mji wa Kasulu mkoani Kigoma kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo kwa wakati.

Katika ziara hiyo Mhe Aweso ametoa maagizo hayo baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo ambapo amesema  kuwa serikali haitavumilia ucheleweshaji wowote wa utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa wananchi huku akimtaka mkandarasi kuongeza kasi na ufanisi maana fedha zipo.

Sauti ya Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso akiwa na viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Isaac Mwakisu, amezungumzia upatikanaji wa huduma ya maji katika wilaya ya Kasulu na namna serikali inavyoendelea kupambana kutatua changamoto ya huduma ya maji katika wilaya hiyo.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Isaac Mwakisu

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wilayani Kasulu, Mhandisi Hussein Nyemba, ameelezea hatua ya mradi huo ulipofikia na namna utakavyokwenda kuwa msada kwa jamii katika halmashauri ya mji wa Kasulu.

Sauti ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wilayani Kasulu, Mhandisi Hussein Nyemba

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kasulu, Mbelwa Chidebwe, ameipongeza serikali kwa juhudi za kupeleka maendeleo kwa wananchi kupitia miradi ya kimkakati kama huo wa maji, akisisitiza kuwa chama hicho kitaendelea kushirikiana na serikali kusukuma mbele maendeleo ya wananchi.

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kasulu, Mbelwa Chidebwe

Wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu wamesema wanatumaini kuwa mradi huo utakapokamilika, utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha hali ya upatikanaji wa maji na kuinua maisha ya wakazi wa mji huo.

Sauti ya Wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila