Joy FM

Vijana, wanawake, ulemavu wapewa mil. 800 Kasulu

23 June 2025, 13:20

Watu wenye ulemavu wakiwa na mgeni rasmi mara baada ya kukabidhiwa hundi ya zaidi ya milion 800 zinazotolewa kwa vikundi

Serikali Wilayani Kasulu imesema itaendelea kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya vikundi vya wenye ulemavu, vijana na wanawake.

Na Emmanuel Kamangu

Halamshauri ya Wilaya ya Kasulu imekabidhi hundi ya zaidi ya shilingi milioni 800 kwa vijana, wanawake  na watu wenye ulemavu katika robo ya tatu na nne ya January hadi june 2024/2025.

Akiwakabidhi hundi hiyo mgeni rasmi wa hafla hiyo, Mbunge wa jimbo la Kasulu  vijijini Bw, Augustine Vuma  amewasihi wanufaika wa mkopo huo kuzitumia fedha hizo vizuri na kurejesha kwa wakati ili kutoa fursa kwa wengine kukopa.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Kasulu  vijijini Bw. Augustine Vuma

Awali mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Halmashauri ya Wilya ya Kasulu Bi, Victoria Moses amesema kwa mwaka wa fedha 2024/25, zaidi ya fedha takribani billion moja zimetolewa kwa vikundi zaidi ya 80 ikiwa ni asilimia 10 ya mapato ya ndani ikilenga kuwakwamua kiuchumi.

Sauti ya Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii halmashauri ya wilya ya kasulu Bi. Victoria Moses
 Mbunge wa Jimbo la Kasulu vijijini Augustini Vuma akiwa na vijana na wanawake ambao ni wanufaika wa mkopo wa asilimia 10 kutoka halmashauri 

Kwa upande wao baadhi ya wanufaika wamesema wanakila sababu ya kuishukuru Serikali kwa kuwapa mikopo nafuu isiyokuwa na riba jambo litakalowafanya kuwa rahisi kuimalika kiuchumi.

Sauto ya baadhi ya wanufaika

Aidha Mwenyekiti wa CCM Wilayani Kasulu Bw, Mbelwa Chidebwe amesema mikopo hiyo ni matokeo mazuri  ya utekelezaji wa ilani ya chama hicho katika kuwavusha kiuchumi  wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.