Joy FM

Serikali kuboresha sera na sheria kwa wenye ualbino

13 June 2025, 17:03

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika maadhimisho ya siku ya watu wenye ualbino Mkoani Kigoma, Picha na Josephine Kiravu

Serikali kuendelea kuboresha sera na sheria kuhusu watu wenye ualbino nchini.

Na Kadislaus Ezekiel

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, amesema Serikali itaendelea kuchukua hatua mahususi kuboresha mifumo ya Kisera na sheria katika kuboresha huduma za watu wenye Ualbino ili kudhibiti ukatili dhidi yao na kuagiza wakuu wa Wilaya kote Nchini, kuhakikisha Jamii ya watu wenye Ualbino inalindwa na kupatiwa huduma zote muhimu kama watu wengine.

 Mheshimiwa Waziri Mkuu Majaliwa, amesema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kukuza uelewa kuhusu Ualbino, mpango unaolenga watanzania kutambua umuhim wao na kushirikishwa katika masuala ya maendeleo.

Sauti ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa watu wenye ualbino katika maadhimisho yaliyofanyika Mjini Kigoma, Picha na Josephine Kiravu

Katika maadhimisho hayo, yamehusisha uzinduzi wa APP ya ALBINO MOBILE, inayolenga kusaidia kutambua Ualbino Walipo maeneo yote Nchini na kuweza kusaidiwa.

Sauti ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa chama cha watu wenye Ualbino Tanzania TASS Godson Mollel, ameomba serikali kuendeela kudhibiti matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye Ualbino, wakati mkuu wa mkoa wa Kigoma Mheshimiwa Thobias Andengenye akiahidi kuendelea kuchukua hatua juu ya usalama wa watu wenye Ualbino na ulemavu.

Sauti ya Mwenyekiti wa chama cha watu wenye Ualbino Tanzania TASS Godson Mollel