Joy FM

Zaidi ya vyandarua milioni 1.7 kusambazwa Kigoma

28 May 2025, 12:18

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali mjini Kigoma wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji wa vyandarua, Picha na Josephine Kiravu

Serikali imesema itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya katika kukabiliana na ugonjwa wa Malaria ambao umekuwa ukisumbumbua katika mataifa mbalimbali kusini mwa jangwa la Sahara.

Na Josephine Kiravu

Zaidi ya vyandarau million 1.7 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 35 vinatarajiwa kusambazwa kwa wananchi Mkoani Kigoma kwa lengo la kupunguza kiwango cha Malaria kutoka assilimia 13%ya sasa hadi kufikia wastani wa Kitaifa ambao ni aslimia 8% ama chini ya wastani huo.

Malaria ni ugonjwa unaozuilika na unaotibika, hata hivyo kila mwaka malaria huwakumba zaidi ya watu milioni 200 na kuua zaidi ya watu laki 600,000 ,na vifo vingi kati ya hivi karibu nusu milioni miomgoni mwao ni watoto wadogo katika bara la Afrika.

Mkuu wa Mkoa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akikata utepe wakati akizindua zoezi la ugawaji vyandarua, Picha na Josephine Kiravu

Katika kukabiliana na tatizo hilo, Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa jeshi la zimamoto na uokoaji Thobias Andengenye amezindua zoezi la usambazaji wa vyandarau zaidi ya  million moja laki saba ambapo amesisitiza matumizi sahihi ya vyandarua hivyo.

Mkuu wa Mkoa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akizungumza wakati akizindua zoezi la ugawaji vyandarua, Picha na Josephine Kiravu
Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali mstaafu wa jeshi la zimamoto na uokoaji Thobias Andengenye

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ugavi kutoka MSD Victor Sungusia amesema watahakikisha kaya zote zilizoandikishwa zinafikiwa na kupatiwa vyandarua.

Sauti ya Mkurugenzi wa Ugavi kutoka MSD Victor Sungusia

Na hapa wananchi wanatoa shukrani zao kwa Serikali huku wanaume wakihamasisha wenzao kutumia chandarua na kwamba si kweli kama vinapunguza nguvu za kiume.

Sauti ya wananchi Kigoma

Zoezi la usambazaji wa vyandarua vyenye dawa ambalo limezinduliwa hii leo linatarajiwa kufikia tamati Juni mosi mwaka huu huku Kauli mbiu ya siku ya Malaria kwa mwaka huu ni Malaria inatokomezwa na sisi,wekeza chukua hatua-Zero malaria inaanza na mimi.

Mkuu wa Mkoa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akikata utepe wakati akizindua zoezi la ugawaji vyandarua, Picha na Josephine Kiravu