Joy FM
Joy FM
22 May 2025, 16:57

Watu wenye mahiataji maalum wakiwemo wenye uoni hafifu wilayani Chamwino mkoani Dodoma wametakiwa kufuatilia na kutambua alama za usalama katika fedha pamoja na utunzaji unaofaa wa fedha.
Na Glory Paschal
Benki Kuu ya Tanzania BoT imetoa elimu ya fedha kwa kundi la watu wenye mahitaji maalum ili waweze kutambua alama za usalama katika fedha wakati wa matumizi katika shughuli zao.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa wa Benki Kuu ya Tanzania BoT, Atifigwege Mwakabalula amesema wameamua kutoa elimu hiyo ili kulisaidia kundi la watu wenye mahitaji maalum yaani uoni hafifu ili waweze kutumia noti za fedha na kuzingatia utunzaji unaofaa.

Katika mafunzo hayo yaliyofanyika wilayani Chamwino mkoani Dodoma Bw. Atifigwege Mwakabalula amesema watu wenye ulemavu au uoni hafifu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za utambuzi wa noti salama kwa kutokuona alama za usalama pamoja na elimu ya fedha.
Aidha katika mafunzo hayo ameeleza majukumu ya Benki Kuu ya Tanzania BoT huku akiwataka kundi hilo linalojulikana kama Tanzania League of Blindness TLB kuendelea kuweka na kutunza fedha katika mazingira salama.