Joy FM

CHADEMA kushushia rungu wanachama wasaliti Kasulu

9 May 2025, 10:45

Viongozi wa chadema wakiwa katika kikao cha baraza la mashauriano wilayani kasulu, Picha na Emmanuel Kamangu

“misingi inayoendelea kuwekwa na chama cha chadema ni misingi inayorudisha uhai wa chama hicho kwa asilimia kubwa”

Na Mwandishi wetu

Chama cha Demokrasia na maendeleo  Chadema wilayani kasulu kupitia Kikao cha baraza la mashauriano  ambacho kimeshirikisha viongozi mbali mbali wa chama wameazimia kuwachukulia hatua wanachama na viongozi wote wilayani humo watakao kisalti chama juu ya agenda yao ya kudai mabadiliko ya mifumo ya uchaguzi .

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kasulu ambaye pia ni diwani wa kata ya mrusi Bw. Fanuel Kisabo pamoja na diwani wa kata ya Nyakitonto Bw, Daniel Nzababa wamesema wataendelea kusimama na chama ili kuhakikisha wanasongambele katika kudai tume huru ya uchaguzi.

Sauti ya Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kasulu ambaye pia ni diwani wa kata ya mrusi Bw. Fanuel Kisabo

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa  Chadema jimbo la kasulu Mjini Bw, Idd  Jafari pamoja na katibu wa chama wilayani humo Bw, Emmanuel Simon wamewaomba wananchi na wanachama  wa chama hicho kuwa wamoja katika kudai mifumo bora ya uchaguzi.

Sauti ya Mwenyekiti wa  Chadema jimbo la kasulu Mjini Bw. Idd  Jafari pamoja na katibu wa chama wilayani humo Bw. Emmanuel Simon

Aidha mwenyekiti wa baraza la wazee wa chama hicho wilayani humo Bw, Gidion Mayani ameiomba serikali kumuachia Mwenyekiti wa chama cha chadema Taifa Tundulisu ili aendelee  kukisimamia chama katika malengo mbali mbali  waliyojiwekea.

Sauti ya mwenyekiti wa baraza la wazee wa chama hicho wilayani humo Bw. Gidion Mayani

Hata hivyo baadhi ya wanachama ambao wameshiriki kikao hicho wamesema misingi inayoendelea kuwekwa na chama cha chadema ni misingi inayorudisha uhai wa chama hicho kwa asilimia kubwa.

Viongozi wa chadema wakiwa katika kikao cha baraza la mashauriano wilayani kasulu, Picha na Emmanuel Kamangu