Joy FM

Watoto 14 wenye utapiamlo wapatiwa dawa lishe Kigoma

28 April 2025, 14:56

Afisa tawala wilaya ya Kigoma Dorah Buzaile, akikabidhi mzigo wa dawa lishe kwa watoto waliogunduliwa kuwa nautapiamlo, Picha na Josephine Kiravu

Serikali imesema itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha tatizo la utapiamlo linaisha kwa watoto.

Na Josephine Kiravu

Watoto wenye umri chini miaka 5 wapatao 14 ambao wamegundulika kuwa na utapiamlo wamepatiwa dawa lishe ikiwemo maziwa na karanga vyenye thamani ya shilingi million 1.8 kwa ajili ya kuboresha afya zao.

Mzazi mwenye mtoto mwenye utapiamlo akiwa amekabidhiwa lishe kwa ajili ya mtoto wake, Picha na Josephine Kiravu

Utapiamlo ni hali ambayo hutokana na kupata chakula ambacho virutubishi vyake havitoshi au viko vingi hadi kusababisha matatizo upande wa afya

Hata hivyo unaweza kuutibu hata kama hauna rasilimali nyingi kwa kumpatia mgonjwa vyakula vingi zaidi na vyenye ubora unaostahili kilishe.

Naye Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mganga Mkuu Manispaa ya Kigoma ujiji, Hashim Mvogogo amewahimiza wazazi kuwa karibu na watoto wao kwa kuhakikisha wanawapatia lishe bora huku akieleza pia namna wanavyowasaidia watoto waliogundulika kuwa na utapiamlo.

Sauti ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mganga Mkuu Manispaa ya Kigoma ujiji, Hashim Mvogogo

Akiwa katika maadhimisho ya siku ya malaria kwa niaba ya mkuu wa wilaya Kigoma, Afisa tawala wilaya ya Kigoma Dorah Buzaile ametumia wasaa huo kuwahimiza wazazi hasa jinsia ya kike kuwa karibu na watoto wao sambamba na kuzingatia lishe ili kuwalinda watoto dhidi ya udumavu.

Sauti ya Afisa tawala wilaya ya Kigoma Dorah Buzaile

Na hapa mmoja wa wazazi ambae anazingatia lishe bora kwa watoto wake anaeleza faida pamoja na urahisi wa kupata lishe bora kwa watoto.

Sauti ya mmoja wa wazazi ambae anazingatia lishe bora kwa watoto wake