Joy FM

Serikali kumaliza mgogoro wa ardhi Kasulu

9 April 2025, 13:20

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Nyumbigwa, Picha na Hagai Ruyagila

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu amewaomba wananchi kutozuia ujenzi wa mradi kwani serikali itahakikisha wanalipwa fidia zao

Na Hagai Ruyagila

Serikali katika halmashauri ya mji Kasulu Mkoani Kigoma imejipanga kumaliza mgogoro wa Ardhi katika kata ya Nyumbigwa kufuatia wananchi kugomea mradi wa ujenzi wa maji taka katika kata hiyo.

Katika mkutano wa wananchi na kamati ya Ulinzi na usalama wilaya ya Kasulu uliofanyikia katika kata ya Nyumbigwa, Baadhi ya wananchi wameomba kulipwa fidia kwenye maeneo yao ambayo utekelezaji wa mradi wa maji taka unaotarajiwa kutekelezwa katika kata hiyo huku wakiomba ushirikishwaji kabla ya mradi kuanza kutekelezwa ili kuepuka migogoro ya ardhi.

Story ya baadhi ya wananchi wameomba kulipwa fidia
Katika mkutano wa wananchi na kamati ya Ulinzi na usalama wilaya ya Kasulu uliofanyikia katika kata ya Nyumbigwa wameomba kulipwa fidia, Picha na Hagai Ruyagila

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Nyumbigwa Benjamini Chalukura ameiomba serikali kufuata utaratibu ili kuwasaidia wananchi ambao mradi huo utapita katika maeneo yao.

Sauti ya Diwani wa Kata ya Nyumbigwa Benjamini Chalukura

Afisa Ardhi halmashauri ya Mji Kasulu Pesha Jackson anasemaje kuhusu eneo hilo?

Sauti ya Afisa Ardhi halmashauri ya Mji Kasulu Pesha Jackson

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl, Vumilia  Simbeye  amesema suala hilo litatafutiwa ufumbuzi kwakuwa dhamira yao ni kuijenga jamii yenye amani na upendo.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia  Simbeye, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl, Vumilia  Simbeye 

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu amewaomba wananchi kutozuia ujenzi wa mradi huo wakati utaratibu wa kuangalia uhalali wa maeneo ya wananchi kulipwa fidia ukiendelea kufanyiwa kazi.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu