Joy FM

Halmashauri ya wilaya ya Kasulu kupokea vyandarua zaidi ya laki 3

14 March 2025, 12:23

Mwakilishi kutoka Wizara ya afya mpango wa taifa wa kudhibiti Malaria Peter Vitanya (NMCP) akitoa elimu kwa wajumbe waliohudhuria kikao cha uhamasishaji kampeni ya kudhibiti ugonjwa wa malaria ,-Picha na Hagai Ruyagila

Halmashauri ya wilaya ya Kasulu inatarajia kupokea vyandarua vyenye dawa bila malipo zaidi ya laki 3 kwa wananchi watakao jiandikisha

Na Hagai Ruyagila

Watendaji wa kata halmashauri ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kusimamia  kampeni ya ugawaji wa vyandarua vyenye dawa katika halmashauri hiyo vyandarua ambavyo vinatarajiwa kutolewa na serikali katika halmashauri hiyo.

Mwakilishi kutoka wizara ya afya  mpango wa taifa wa  kudhibiti Malaria Peter vitanya (NMCP)amebainisha hayo wakati  akitoa elimu maalumu kwenye kikao cha uhamasishaji wa  kampeni ya ugawaji wa vyandarua vyenye dawa kwenye kaya kwa mkoa wa Kigoma.

Amesema ugawaji wa vyandarua bila malipo unatarajiwa katika halmashauri zote za Mkoa wa Kigoma ili kuhakikisha jamii inakuwa salama na kupunguza  maambukizi ya ugonjwa wa Malaria.

Sauti ya Peter Vitanya mwakilishi wa kutoka wizara ya afya

Kaimu mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Kasulu Bw.Komesha kaminyoge amesema halmashauri inatarajia kupokea zaidi ya vyandarua laki 3 na vitatolewa kwa wananchi watakao jiandikisha huku akisisitiza matumizi sahihi ya vyandarua hivyo.

Sauti ya Kaimu mkurugenzi Kasulu DC 

Hata hivyo mratibu wa malaria katika halmashauri hiyo Berlino Mlange amesema halmashauri ya wilaya ya kasulu imefikia asilimia 37 ya maambukizi ya ugonjwa wa Malaria huku mkoa wa Kigoma ukiwa ni asilimia 13 za maambuzi ya ugonjwa huo  hivyo ameeleza kuwa wanaendelea kuweka mikakati kuhakikisha kila kaya inapata chandarua ili kukabiliana kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria

Sauti ya mratibu wa malaria Berlino Mlange
Wshiriki,Viongozi pamoja na watoa elimu ya kudhibiti ugonjwa wa malaria ,-Picha na Hagai Ruyagila