Joy FM

NEMC yagawa miti kwa shule tano Kigoma

7 March 2025, 09:43

Baadhi ya maafisa wa NEMC wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi shule ya Alpha baada ya kugawa miti kwa shule tano za wilaya Kigoma, Picha na Timotheo Leonard

Jamii mkoani Kigoma imeaswa kuwa na desturi ya kupanda miti ili kusaidia kuendelea kutunza mazingira na kupunguza mabadiliko ya tabianchi.

Na Timotheo Leonad

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Kanda ya Magharibi, imegawa miti zaidi ya elfu moja kwa shule tano za wilaya ya Kigoma lengo likiwa ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira.

Wanafunzi wa shule ya Alpha wakipanda miti baada ya kugawiwa na NEMC ili kutunza mazingira, Picha na Timotheo Leonard

Kauli hiyo imetolewa na Edith William Makungu ambaye ni Afisa Mwandamizi kutoka NEMC Kanda ya Magharibi wakati wa ugawaji wa miti kwa shule mbalimbali ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Amesema malengo ya kugawa miti kwa shule hizo ni kuwawezesha watoto wakiwa bado wadogo kufahamu umuhimu wa upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwa kukabiliana na mabadiliko ya  tabianchi.

Sauti ya Edith William Makungu Afisa Mwandamizi kutoka NEMC Kanda ya Magharibi
Afisa kutoka NEMC akimwagilia maji mti uliopandwa na wanafunzi wa shule ya Alpha, Picha na Timotheo Leonard

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Alpha Adventist Pre and Primary school Mwalimu James Chirstopher ameahidi kuitunza miche hiyo huku akiipongeza serikali kwa kuwapatia miti hiyo.

Sauti ya Mkuu wa Shule ya Alpha Adventist Pre and Primary School Mwalimu James Chirstopher

Baadhi ya wanafunzi waliokabidhiwa majukumu ya kuitunza miti hiyo wameipongeza NEMC na kuahidi kuitunza miti hiyo ili kutunza mazingira na kuhakikisha inasaidia kupata hewa safi wakiwa mazingira ya shuleni.

Sauti ya baadhi ya wanafunzi waliokabidhiwa majukumu ya kuitunza miti hiyo wamekiipongeza NEMC na kuahidi kuitunza miti hiyo
Afisa Mwandamizi kutoka NEMC kanda ya Magharibi Edith William Makungu akipanda mti, Picha na Timotheo Leonard