Joy FM

TEA yakabidhi mradi wa nyumba nne na madarasa matatu Kasulu

26 February 2025, 14:38

Muonekano wa madarasa yaliyokabidhiwa baada ya kukamilika, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imeendelea kuboresha elimu nchini kwa kujenga vyumba vya madarasa ili wananfunzi waweze kupata elimu bora.

Na Hagai Ruyagila

Mamlaka ya Elimu Tanzania TEA imekabidhi mradi wa nyumba nne kwa shule ya sekondari Nyumbigwa na madarasa matatu katika shule ya Msingi Msivyi halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma yenye thamani ya shilingi milioni 160 ili kurahisisha mfumo wa utoaji elimu kwa wanafunzi na waalimu kuwa rahisi kwenye ufundishaji na ujifunzaji.

Hayo yamebainishwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya mamalaka ya elimu Tanzania (TEA) Paulo Kawawa ambaye ni afisa elimu miradi wa mamlaka ya elimu Tanzania amesema miradi hiyo imejengwa kuanzia mwaka wa fedha 2020 / 2021, 2021 / 2022, 2022 / 2023 na 2023 /2024 na lengo la serikali  ni kutoa msaada unaoenda kurahisisha utoaji wa elimu katika suala la ufundishaji na ujifunzaji.

Sauti ya mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya mamalaka ya elimu Tanzania (TEA) Paulo Kawawa
Mwakilishi Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya mamalaka ya elimu Tanzania (TEA) Paulo Kawawa akiwa kwenye picha na baadhi ya viongozi wakati wa kukabidhi mradi

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Msivyi Metusela Maliatabu amesema kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo umesaidia kuongeza ufaulu na kupunguza utoro kwa wanafunzi wa shule hiyo japo bado kuna changamoto zinazo endelea kuikabili shule hiyo ikiwemo uhaba wa madarasa na nyumba za waalimu.

Sauti ya Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Msivyi Metusela Maliatabu

Diwani wa kata ya Muganza Ezron Budulege ameishukuru serikali kwa namna ilivyosaidia shule hiyo kupata madarasa matatu ambayo yatapunguza changamoto ya miundombinu shuleni hapo.

Sauti ya Diwani wa kata ya Muganza Ezron Budulege

Nao baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Msivyi wamezungumzia namna bora ambayo serikali imepunguza changamoto katika shule hiyo katika suala zima la ujifunzaji shuleni hapo.

Sauti ya baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Msivyi
Muonekano wa darasa lililokabidhiwa na TEA, Picha na Hagai Ruyagila