Joy FM

Diwani atoa msaada wa madawati kwa shule sita Kasulu

6 February 2025, 11:56

Diwan kisabo akimkabidhi dawati 30 kaimu mkuu wa shule ya mkombozi Bi Aziza Bakali, Picha na Emmanuel Kamangu

Wadau mbalimbali wa maendeleo wametakiwa kuwa na desturi kuchangia kwenye maendeleo ya shule ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingira mazuri na kuongeza ufaulu

Na Emmanuel Kamangu

Jumla ya madawati 210 yenye thamani ya zaidi ya milioni 11 zimetengenezwa na diwani  wa kata ya mrusi halmashauri ya mji wa kasulu Bw, Fanuel kisabo na kuzigawa kwa shule  sita za msingi za kata hiyo ndani ya miaka mitano.

Akizungumza katika hafla ya kugawa  dawati 110 diwani kisabo amesema dawati hizo zinatimiza jumla ya dawati 210 ambazo amezigawa kwa shule sita za msingi za kata ya mrusi toka mwaka 2020 hadi sasa nakuomba wadau wengine wa maendeleo kuendelea kusaidiana kutatua kero ya uhaba wa madawati katika kata hiyo.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi mkombozi, Bajana, ndalichako, Juhudi, kasulu na shule msingi Mrusi, Picha na Emmanuel Kamangu.
Sauti ya Diwani wa kata ya Mrusi Bw. Fanuel kisabo

Aidha Diwani kisabo amesema ni wakati wa kufanya kila jitihada ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingra rafiki yatakayo wasaidia kufanya vizuri katika masomo yao.

Sauti ya Diwani wa kata ya Mrusi Bw. Fanuel kisabo

Kwa upande wao baadhi ya wakuu wa shule za msingi katika kata hiyo mmoja wao akiwa Bi,Pendo Nkuba wakipokea dawati hizo wamesema zitasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua kero ya baadhi ya watoto kusoma wakiwa wamekaa chini.

Sauti ya baadhi ya wakuu wa shule za msingi katika kata hiyo mmoja wao akiwa Bi. Pendo Nkuba

Katika shule sita za msingi za kata ya mrusi kuna jumla ya wanafunzi 7707  huku shule zote hizo zikikabiliwa na  upungufu wa madawati 995.

Diwani wa kata ya Mrusi Bw, Fanuel kisabo, Picha na Emmanuel Kamangu