Joy FM

Watumishi wa umma watakiwa kuzingatia utawala bora Buhigwe

31 January 2025, 13:07

Washiriki wa mafunzo ya utawala bora yaliyotolewa kwa watumishi wa umma Wilayani Buhigwe, Picha na Emmanuel Kamangu

Watumishi wa umma Wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia utawala bora ili kuhakikisha wanafikia azma ya kufikisha maendeleo kwa wananchi.

Na Emmanuel Kamangu

Katibu tawala wa Wilaya ya Buhigwe Utefta Mahega amewataka Watumishi wa umma Wilaya ya Buhigwe kuzingatia Demokrasia na Utawala bora ili kuendelea kujenga imani kwa Wananchi dhidi ya Serikali yao ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Bi Mahega amesema hayo katika mafunzo ya Elimu ya Uraia na Utawala bora ambayo yameandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria Kwa watalamu mbali mbali  katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe yakilenga kutoa ufahami katika kuhakikisha wanasimaia haki na sawa katika jamii.

Sauti ya Katibu tawala wa Wilaya ya Buhigwe Utefta Mahega

 Aidha Bi Joyce Mushi ambaye ni Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria na Mratibu wa mafunzo hayo amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo viongozi wa Serikali za Mitaa ili kutatua changamoto na malalamiko katika jamii kwa kuzingatia demokrasia.

Joyce Mushi ambaye ni Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Picha na Emmanuel Kamangu
Sauti ya Joyce Mushi ambaye ni Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe NGeorge Emmanuel Mbilinyi ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuleta mafunzo hayo na kuwasihi watumishi hao kutumia mafunzo hayo katika utendaji wao wa kazi. 

Sauti ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe NGeorge Emmanuel Mbilinyi

Hata hivyo baadhi ya watenji wa kata na vijiji ambao wameshiriki mafunzo hayo wamesema yatawasaidia Kwa kiasi mkubwa kuendelea kusimamia haki na utawala  bora katika  jamii.