Joy FM

TAKUKURU Kigoma yabaini mapungufu miradi 31 ya maendeleo

31 January 2025, 11:25

Naibu mkuu TAKUKURU mkoa wa kigoma John Mgallah akizungumza na wandishi wa habari,-Picha na Orida Sayon

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Kigoma imebaini mapungufu madogo madogo katika miradi 31 ya maendeleo kati ya miradi 32.

Na Orida Sayon

Akitoa taarifa ya ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha kuanzia mwezi wa oktoba hadi Disemba 2024, Naibu Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa kigoma John Mgallah  amesema kuwa taasisis hiyo imefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 32 yenye thamani ya Tsh. 11,453,699,642.67/=

Sauti ya Naibu mkuu TAKUKURU

Mgallah amesema miongoni mwa miradi yenye mapungufu ni  katika ujenzi bweni 1, madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo katika shule ya Sekondari Nyarubanda yenye thamani ya Mil.341,600,000/= kama anavyoeleza

Sauti ya Naibu mkuu TAKUKURU

 Baadhi ya wananchi mkoani Kigoma wametoa maoni yao juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kwamba  imekua ikicheleweshwa kukamilika kwa wakati  huku mingine ikikamilika haipo kwenye ubora wake na kuomba serikali kuchukulia hatua wote wanaohusika na ucheleweshwaji wa miradi hiyo.

Sauti ya wananchi mkoani Kigoma

Kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu ;tutimize wajibu