Joy FM
Joy FM
21 March 2026, 12:40

Takribani wananchi elfu 32 kutoka vijiji vya Kata ya Kagerankanda Halmashauri ya Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma wanatarajia kupata huduma za afya karibu baada ya Serikali kujenga kituo cha afya katika kata hiyo ambacho kipo mbioni kuanza kutoa huduma kwa wananchi
Na Tryphone Odace
Wananchi wa Kijiji cha Kagerankanda Halmashauri ya Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma wamepongeza serikali kwa kujenga kituo cha afya na hali itakayosadiai kupunguza vifo na kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta huduma za afya katika maeneo mengine.

Wakizungumza na Redio Joy Fm ilipotembelea kijiji cha Kagerankanda wananchi hao wamesema licha ya uwepo wa zahanati walilazimika kwenda kutafuta huduma za afya nje ya kata yao hali iyosababisha kutumia gharama kubwa na wakati mwingine wajawazito kujifungulia njiani kutokana na umbali mrefu.

Naye Afisa Mfawidhi wa Zahanati ya Kagera nkanda ambaye pia ndiye msiamamizi wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha afya Kagerankanda Richard Joseph Marwa amesema ujenzi wa kituo hicho utakapokamilika utasaidia kuhudumia jumla ya wananchi elfu 32 kutoka katika vijiji vya kata hiyo.
Akizungumzia huduma zinazotolewa kwa sasa katika zahanati Kagerankanda amesema kutokana na wingi wa wananchi wa kata hiyo zahanati hiyo ililazimika kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha wanapunguza wimbi wa wagonjwa waliokuwa wakipata hudam katika zahanati hiyo.

Diwani wa Kata ya Kagerankanda Yohana Mwilabule amesema ujio wa kituo hicho kutasaidia kuongeza upatikanaji wa huduma muhimu za afya kwa wananchi ambapo ameomba serikali kuhakikisha kinakamilika kwa haraka ili waaanze kupata huduma.

Kwa upande wake, Afisa mtendaji wa Kata ya Kagerankanda Banyukwa John Makinga ameeleza kuwa ujenzi huo ulishirikisha wananchi na kufanikiwa kuanza ujenzi wa mradi ambao unaenda sasa kumaliza kilio cha wananchi kukosa huduma muhimu za afya.