Joy FM

Wananchi waomba TBS kudhibiti bidhaa zisizo na ubora Kigoma

11 March 2026, 17:16

Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon, Picha na Lucas Hoha

Udhibiti wa bidhaa szisizo na ubora husaidia kulinda afya na usalama wa wananchi na mara nyingi bidhaa hizo kama dawa, vipodozi na vyakula ambavyo hutengenezwa bila kufuata viwango vya ubora unaotakiwa.

Na Lucas Hoaha

Wananchi Mkoani Kigoma wameomba Shirika la viwango Tanzania (TBS) kudhibiti bidhaa ambazo hazina ubora zinazotengenezwa viwandani ili kuepuka athari zitokanazo na bidhaa hizo ikiwemo kupata kansa ya ngozi

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema TBS wanakila sababu ya kudhibiti bidhaa hizo kwa kufanya misako ya mara kwa mara hasa viwandani ili kubaini ubora wa bidhaa kabla ya kuwafikia watumiaji.

Sauti ya wananchi Kigoma

Awali akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon amesema tangu kuanzishwa kwa shirika hilo kanda ya magharibi wamefutilia viwanda vikubwa na vidogo 129 na kutoa leseni kwa viwanda hivyo, huku akifafanua namna wanavyofuatilia majengo yakuhifadhia chakula.

Sauti ya Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon
Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon, Picha na Lucas Hoha

Aidha amesema shirika hilo limekuwa likifuatilia bidhaa amabazo ni hafifu zilizopo sokoni na pindi wanapozibaini wamekuwa wakiziteketeza kwa moto ili kuondoa madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi.

Sauti ya Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon
Meneja Shirika la Viwanga Tanzania TBS Kanda ya Magharibi Hamis Seleleko Simon, Picha na Lucas Hoha

Shirika la viwango Tanzania TBS Kanda ya Magharibi limekuwa likifanya kazi  ya kukagua bidhaa hafifu kwenye mikoa mitatu yaani Kigoma, Katavi na Tabora ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua dhidi ya watu wanaohusika kuingiza bidhaa hizo nchini.