Joy FM

Wananchi kunufaika na bima ya afya Kasulu

6 March 2026, 16:30

Mkuu wa Wilaya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu akikabidhi kadi ya bima ya afya kwa mnufaika, Picha na Hagai Ruyagila

Bima ya afya kwa wote ni mpango unaolenga kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma za matibabu bila kuathiriwa na gharama za matibabu hii ni baada ya serikali kuimarisha mfumo wa bima ya afya ili kuwasaidia wananchi kupata huduma bora za afya.

Na Hagai Ruyagila

Zaidi ya Wananchi 20,000 wanaotoka katika familia zenye uhitaji maalumu Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wameanza kunufaika na kadi za bima ya afya zinazotolewa na serikali ambazo zitawawezesha kupata huduma za matibabu bila kulipia gharama yoyote.

Wananchi ambao ni wanufaika wa mpango wa bima ya afya kwa wote, Picha na Hagai Ruyagila

Akizindua rasmi zoezi hilo katika ofisi ya Mtaa wa Nyarumanga, Kata ya Kigondo Halmashauri ya Mji Kasulu, Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu, amesema mpango huo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu,

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Mh, Ayubu Ngalaba amewatoa hofu wananchi ambao bado hawajapata bima kuwa na subira kwasababu zoezi hilo bado linaendelea.

Sauti ya Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Mh, Ayubu Ngalaba
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Mh, Ayubu Ngalaba, Picha na Hagai Ruyagila

Meneja wa NHIF Mkoa wa Kigoma Gwamaka Mwakyoma amesema wamekuja kutekeleza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuhakikisha wananchi wanapatiwa matibabu kama Rais alivyosema.

Sauti ya Meneja wa bima ya Afya mkoa wa Kigoma Gwamaka Mwakyoma
Meneja wa NHIF Mkoa wa Kigoma Gwamaka Mwakyoma, Picha na Hagai Ruyagila

Baadhi ya wananchi walionufaika na fursa hiyo wameishuruku serikali kwa kuwawezesha kupata Bima za afya ambazo zinaenda kurahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa urahisi.

Sauti ya Baadhi ya wananchi walionufaika