Joy FM
Joy FM
23 February 2026, 12:37

Watoto ni hazina ya taifa na msingi wa maendeleo ya baadaye ya jamii yoyote hivyo wanahitaji malezi bora, elimu, ulinzi na mazingira salama ili waweze kukua kimwili, kiakili na kimaadili licha ya kuwa bado kuna changamoto ya watoto kutumikishwa kwenye shughuli za biashara wakiwa chini ya umri unaoruhusiwa kisheria.
Na Michael Mpunije
Jeshi la Polisi dawati la Jinsia na Watoto Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaondoa Watoto wanaofanya shughuli za biashara chini ya umri wa miaka 18 ukiwa ni mkakati wa kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya Watoto.
Akizungumza na wananchi wa kata ya Murusi, Mkuu wa dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Kasulu Inspekta Maimuna Omary amesema zoezi hilo litakuwa endelevu ili kuhakikisha Watoto wanaofanya shughuli hizo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo wanachukuliwa hatua za Kisheria.

Amewataka wazazi na walezi kushirikiana katika suala la Malezi kwa kutimiza wajibu wao kwa Watoto ikiwa ni Pamoja na kuwaandikisha shuleni Watoto wote wenye umri wa kuanza masomo.
Afisa ustawi wa jamii Halmashauri ya mji Kasulu, Tausi Baraka ameitaka jamii kushirikiana kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na Ukatili kwa kwa Watoto kwa kutoa taarifa za vitendo hivyo kwenye mamlaka husika ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa wote watakaobainika.
