Joy FM

Migogoro ya familia inavyoathiri maendeleo ya ukuaji kwa watoto

28 January 2026, 15:04

Baadhi ya aafisa kutoka Manispaa ya Kigoma ujiji wakiwa katika studio za Joy Fm katika kipindi cha Goodmorning Kigoma, Picha na Hamis Ntelekwa

Familia ni msingi muhimu sana katika malezi na ukuaji wa mtoto kwani mtoto hupata upendo, ulinzi, maadili na mwelekeo wa maisha, hata hivyo, pale migogoro inapojitokeza mara kwa mara ndani ya familia, huathiri vibaya maendeleo ya ukuaji wa mtoto katika nyanja mbalimbali za maisha yake.

Na Orida Sayon

Migogoro ya ndoa kati ya baba na mama katika familia imeelezwa kuwa changamoto inayoathiri maendeleo ya ukuaji wa mtoto kijamii, kihisia, kisakolojia na kitabia.

Hayo yameelezwa na Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya kigoma ujiji, Eliud Galkan wakati akizungumza na Joy Fm ambapo ameeleza kuwa asilimia kubwa migogoro ya ndoa katika familia imekuwa ikisababisha matokea hasi yanayoathiri maendeleo ya makuzi ya watoto.

Sauti ya fisa maendeleo ya jamii Manispaa ya kigoma ujiji, Eliud Galkan

Kwa upande wake, Afisa ustawi wa jamii Mfawidhi Epheta Msiga amesema mila na desturi za jamii zetu zimekua chanzo cha migogoro ya ndoa kwa kuchochea ndoa katika umri mdogo.

Sauti ya Afisa ustawi wa jamii Mfawidhi Epheta Msiga

Aidha Kaimu Afisa Dawati la jinsia na watoto Kigoma Diana Kadigi ameitaka jamii kutatua changamoto zinazotokana na migogoro ya ndoa na kudai kuwa ni chanzo cha kuondoa upendo na amani katika jamii.

Sauti ya Kaimu Afisa Dawati la jinsia na watoto Kigoma Diana Kadigi

Kukumbuka kuwa mtoto ni taifa la kesho anapaswa kulindwa , kupewa haki ya malezi chanya , kuheshimu haki za mtoto na kutoshirikishwa katika migogoro ya kifamilia ili kumjenga kihisia , kisaikolojia, na kijamii katika malezi na ,makuzi.