Joy FM

Mvua yaharibu nyumba, mali Itebula Uvinza

26 January 2026, 15:50

Ni wananchi wa Kata ya Itebula wakiwa wamekaa nje baada ya mvua kuezua nyumba zao, Picha na Sofia Cosmas

Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Kata ya Itebula Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma wameomba serikali na wadau kuwasaidia baada ya nyumba zao kuezuliwa na mvua iliyoambatana na upepo na kusababisha nyumba na mali zao kuharibika.

Na Timotheo Leonard

 Mvua kubwa iliyonyesha ikiambatana na upepo mkali  katika Kijiji cha Itebula Kata ya itebula Halmashauri ya wilaya ya uvinza Mkoani Kigoma, imesababisha madhara kwa wananchi wa eneo hilo ambapo nyumba zaidi ya ishirini zimeezuliwa na upepo na kuwaacha bila makazi ya kuishi.

Muonekano wa nyumba iliyoezuliwa na mvua katika Kata ya Itebula Wilayani Uvinza, Picha na Sofia Cosmas

Protas  Guzuye ambaye ni Mtendaji wa Kiijiji cha itebula kata ya Itebula akizungumza na Radio Joy fm kwa njia ya simu, amesema chanzo cha kuezuliwa kwa nyumba hizo ni mvua iliyoambatana na upepo mkali na kusisitiza wananchi kupanda miti ili kupunguza madhara.

Sauti ya Protas  Guzuye ambaye ni Mtendaji wa Kiijiji cha itebula kata ya Itebula

Kwa upande wake , Batromeo Sigaya mwenyekiti  wa Kitongoji cha Chemchem kata ya Nguruka yeye anasimlia namna mvua ilivyoanza kunyesha   kwa karibu saa moja na kwamba wananchi hawanabudi kuzingatia ubora wakati wa ujenzi wa nyumba zao.

Miongoni mwa nyumba zilizoezuliwa na mvua katika kata ya Itebula Wilyani Uvinza Mkoani Kigoma, Picha na Sofia Cosmas
Sauti ya Batromeo Sigaya mwenyekiti  wa Kitongoji cha Chemchem kata ya Nguruka

Baadhi ya wakazi wa kata ya itebula Tarafa ya Nguruka Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza wameiomba serikali kuendelea kushikamana na wananchi waliopata madhara kutokana na mvua hiyo.

Sauti ya baadhi ya wakazi wa kata ya Itebula Tarafa ya Nguruka Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza
Miongoni mwa nyumba zilizoezuliwa na mvua katika kata ya Itebula Wilyani Uvinza Mkoani Kigoma, Picha na Sofia Cosmas

Aidha mamlala ya hali ya hewa nchini Tanzania TMA inaendelea kusisitiza wananchi kuchukua tahadhari za mvua pamoja na kufuatilia utabiri wa hali ya hewa wakati wote ilikuepuka madhara yanayoweza kuepukika.

Muonekano wa nyumba iliyoezuliwa na mvua katika Kata ya Itebula Wilayani Uvinza, Picha na Sofia Cosmas