Joy FM

Mikopo ya 10% ilivyoinua maisha ya wananchi Kigoma

9 January 2026, 11:53

Baadhi ya maafisa maendeleo walipotembelea vikundi vinavyonufaika na mikopo ya Halmashauri, Picha na Orida Sayon

Mikopo ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika kujenga maisha bora na kuchangia maendeleo endelevu.

Na Orida Sayon

Baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji hasa vijana wameomba kuendelea kupewa elimu ya mikopo ya asilimia 10 kutoka katika mapato ya halmashauri.

Wameeleza hayo wakati wa mazungumzo na kituo hiki mazungumzo yaliyolenga kufahamu ni upi uelewa wa makundi ya wanawake, vijana, wazee na wenye ulemavu kuhusu mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri mbalimbali hapa nchini.

Baadhi ya wanakikundi cha Womens and Children Group ambao ni wanufaika wa mikopo, Picha na Orida Sayon

Na hapa Joy Fm, inafika katika moja ya kikundi cha Womens and Children Group ili kujua wameweza je kufikia hatua ya kupata mkopo kutoka halmashauri na vijana ambao bado hawajapata mikopo kujua uelewa wao na hapa wanaeleza.

Sauti ya wananchi wanufaika wa mkopo

Naye Afisa maendeleo kutoka Manispaa ya Kigoma Ujiji Jabir Majira amesema serikali imeendelea kutoa mwongozo na elimu ya namna ya kupata mikopo hiyo pamoja na namna ya kutumia, kusimamia na kuendesha miradi akidai awamu ya kwanza serikali ilipata hasara kwa baadhi ya makundi kushindwa kurejesha.

Afisa maendeleo kutoka Manispaa ya Kigoma Ujiji Jabir Majira akiwa na maafisa wengine walipotembelea vikundi, Picha na Orida Sayon
Sauti ya Afisa ya maendeleo

Aidha Bw. Majira amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 Manispaa ya Kigoma Ujiji wametenga milioni 500 kwa ajili ya makundi yay a wanawake, vijana ,wazee na watu wenye ulemavu

Sauti ya Afisa maendeleo kutoka Manispaa ya Kigoma Ujiji Jabir Majira