Joy FM

Pikipiki 6 zakabidhiwa kwa wajasiriamali Kigoma

24 December 2025, 09:12

Pikipiki ambazo zimetolewa kwa vikundi vya wajasiriamali ikiwa ni sehemu ya mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya Halmashauri

Serikali imesema itaendelea kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu huku ikisisitiza waliopata mkopo kuzitumia kwa manufaa na kurejesha kwa wakati

Na mwandishi wetu

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, imekabidhi pikipiki sita kwa vikundi viwili vya wajasiriamali ikiwa ni sehemu ya mkopo wa 10% kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Katibu tawala Wilaya Kigoma akikabidhi pikipiki kwa mwakilishi wa kikundi mojawapo kilichopata mkopo wa pikipiki

Pikipiki hizo zimekabidhiwa kwa wajariamali hao na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigoma Mganwa Nzota zenye thamani ya shilingi milioni 21.5 zikiwa na bima kubwa ya kukabiliana na majanga.

Aidha Mganwa Nzota amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kusimamia pikipiki hizo ili kuwanufaisha na kuwainua kiuchumi kwa kuwapatia madereva wenye mafunzo ya udereva na Lesseni.

Baadhi ya vijana waliopatiwa mkopo wa pikipiki Manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Mwandishi wetu

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Lawi Kajanja amesema Halmashauri inaendelea kutenga mapato ya asilimia 10 ili kuendelea kuinua uchumi wa wananchi kupitia mikopo isiyokuwa na riba.

Vikundi vilivyonufaika na mkopo huo wa pikipiki ni Kikundi cha wanawake cha Chapa kazi kilichopo Kata ya Businde kilichopokea pikipiki tatu na kikundi cha vijana cha Kazi na maendeleo kilichopo Kata ya Mwanga Kusini kikipokea pikipiki tatu.

Katibu tawala Wilaya Kigoma akizungumza mara baada ya kukuabidhi mkopo wa pikipiki kwa vikundi, Picha na Mwandishi wetu

Utoaji wa mikopo hiyo isiyokuwa na riba Manispaa ya Kigoma Ujiji ni awamu ya pili ambapo vikundi sitini na Sita vinakuwa vimenufaika kwa zaidi ya fedha za iitanzania milioni mia iita kumi na Sita.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma ujiji akisalimiana na mwakilishi wa kikundi mojawapo kilichopata mkopo wa pikipiki, Picha na Mwandishi wetu