Joy FM

SHIMKIATA yakuza mila, tamaduni za asili kwa jamii Kigoma

23 December 2025, 11:48

Wana ushirika wa ibada wakiwa katia wakisali Patatu wakati wa ibada ya Elombe, Picha na Tryphone Odace

Asili na jadi ni msingi wa kukuza, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni na mila kwa kuzithamini na kuzifundisha kwa vizazi vipya na kuhakikisha jamki inabaki na utambulisho imara huku ikikua na kubadilika katika njia chanya.

Na Tryphone Odace

Wito umetolewa kwa jamii mkoani Kigoma kuendelea kuwafundisha vijana mila, utamaduni na desturi za jamii husika kama njia ya kuchochea maendeleo na utu kwa jamii.

Hayo yameelezwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Kigoma Ujiji, Aida Nzowa wakati wa ibaada ya kiasili ijulikanayo kama Elombe ambayo hufanyika mara moja kwa mwaka kwa kuwakutanisha watu kutoka maeneo mbalimbali  duniani.

Amesema ibaada ya jadi na asili ambayo ipo chini ya shirika la maendeleo ya kijamii katika asili na tamaduni (SHIMKIATA) ni muhimu kuendelea kuenziwa kwani inasaidia jamii kurudi kwenye misingi ya upendo na mshikamano na kusaidia watu kutofanyiana mambo mabaya.

Sauti ya Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Kigoma Ujiji, Aida Nzowa
Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Kigoma Ujiji, Aida Nzowa akizungumza wakati wa ibaada ya asili inafanywa na SHIMKIATA ili kukuza tamaduni za asili kwa jamii

Katika maendeleo ya sasa ambayo yamekuwa yakibadilika kila kukicha ni muhimu kukieleza kizazi cha sasa na kesho ili kiweze kukua kikifahamu na kutambua kuwa mila, asili na utamaduni ni nguzo muhimu sana katika kubadilisha jamii kuachana na vitendo viovu.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi, Mwakilishi wa kamati ya maandalizi ya ibada hiyo Muntu Bhabhantu amesmea lengo lao ni kujenga jamii yenye mshikamo kupitia asili na tamaduni.

Sauti ya Mwakilishi wa kamati ya maandalizi ya ibada hiyo Muntu Bhabhantu
Wana ushirika wa ibada wakiwa katia wakisali Patatu wakati wa ibada ya Elombe, Picha na Tryphone Odace

Kwa upande wake, Kiongozi wa wanajadi duniani Mwami Lokoko amesema jadi ina muhimu katika kuwasaidia watu kutambua chimbuko lao na misingi ya kale.

Sautu ya Kiongozi wa wanajadi duniani Mwami Lokoko
Kiongozi wa wanajadi duniani Mwami Lokoko akiwa amewasilikatika ibada ya jadi, Picha na Tryphone Odace

Mwami Lokoko, amesema wataendelea kufundisha kueleza umma ili uweze kufahamu na kutambua asili na jadi yao ilivyo ili iweze kuwasaidia kuishi katika misingi ya kusaidiana na kutokengeuka na kuhadaliwa na ulimwengu wa sasa.

Msaada uliotolewa na vija wa Kitongoni Jogging wakimkabidhi zawadi kiongozi wa jadi duniani Mwani Lokoko, Picha na Tryphone Odace

Baadhi ya wananchi na viongozi wa kata ya Kitongoni Manispaa ya Kigoma Ujiji, walihudhuria ibada hiyo wamesema jamii kufundishwa jadi kupitia asili na tamaduni zao inasaidia kupunguza watu kufanya matendo maovuikiwemo ukatili.

Sauti ya Baadhi ya wananchi na viongozi wa kata ya Kitongoni
Kiongozi wa wanajadi duniani Mwami Lokoko akiwa amewasilikatika ibada ya jadi, Picha na Tryphone Odace
Afisa maendeleo ya jamii Aida Nzowa akipokea hundi iliyotolewa na SHIMKIATA kwa ajili ya watu wenye uhitaji, Picha na Tryphone Odace

Ibaada hiyo imeenda sambamba na utoaji wa misaada kwa wasiojiweza, kufungisha ndoa mbili za kimila ikiwa chini ya kaulimbiu isemayo “Elombe ni urithi wetu, Amani yetu, Umoja wetu, Faraja kwa wenzetu kwa maendeleo endelevu.