Joy FM

Wahitimu UBA waaswa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari Kigoma

19 December 2025, 13:03

Pichani ni Mkuu wa maudhui mtandaoni kutoka kampuni ya Azam media akiwa watumishi wachuo cha UBA, Picha na Orida Sayon

Wahitimu na wanafunzi wa vyuo mbalimbali nchini wanaosoma fani ya uandishi wa habari, wameshauriwa kuongeza ujuzi wao katika masuala ya kidijitali, ili kuepusha matumizi mabaya ya teknolojia yanayoweza kupotosha umma.

Na Orida Sayon

Wahitimu kutoka chuo cha utangazaji Ujiji Broadcasting Academy (UBA) wametakiwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yao kuongeza ujuzi wao katika masuala ya kidijitali, ikiwemo matumizi sahihi ya akili mnemba (AI).

Amesema hayo Mkuu wa maudhui mtandaoni kutoka kampuni ya Azam media na mjumbe wa bodi ya chuo cha UBA  Hassan Mhelela amesema hayo wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Anglikana uliopo Mjini Kigoma.

Wahitimu waliohitimu katika cha Ujiji Broadcasting Academy (UBA) wakiwa kwenye picha ya pamoja, Picha na Orida Sayon

Mhelela amesema soko la ajira linahitaji wataalamu wanaozingatia kanuni na maadili ya habari ambayo yanarahisisha ufanyaji kazi.

Mkuu wa chuo cha UBA Bi. Victoria Ndekeye anaeleza namna wanavyowandaa wanafunzi wao kuhakikisha wanazingatia kanuni na maadili ya taaluma yao hasa katika matumizi ya teknolojia.

Na baadhi ya Wahitimu wakawa na haya ya kueleze kuhusu matumizi ya akili mnemba na faida za maadili ya uandishi katika majukumu yao.

Mkuu wa chuo cha UBA Victoria Ndekeye akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa Redio Joy Fm Maria Buremo walipohudhuria mahafali ya kwanza ya chuo hicho, Picha na Orida Sayom