Joy FM

Kibondo, Uvinza zatolewa mashindano ya ujirani mwema Burundi

16 December 2025, 13:15

Mkuu wa Mkoa Burungu nchini Burundi Parfait Mboninyibuka (kulia) akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa mashindano ya ujirani mwema Maarufu kama Lake Tanganyika Cup baina ya timu za Kombaini za Wilaya za Mkoa Kigoma na Kombaini za mikoa ya Burundi (kushoto) Wilfred Lutera mjumbe wa Kamati ya mashindano kutoka ofisi ya Mkuu Mkoa Kigoma, Picha na Mwandishi wetu

Mashindano ya ujirani mwema yaliyokuwa yanaendelea katika Wilaya ya Makamba Nchini Burundi Timu kutoka Mkoa wa Kigoma Tanzania zimetolewa kwa kipigo

Na Mwandishi wetu Burungu, Burundi

Timu za wachezaji mchanganyiko za wilaya za Kibondo na Uvinza za mkoani Kigoma nchini Tanzania zimeyaaga mashindano ya ujirani mwema yanayofanyika wilaya ya Makamba mkoa Burungu nchini ambapo timu nne za Tanzania na nne za Burundi zinashiriki mashondano hayo yanayoendeshwa kwa njia ya mtoano.

Uvinza imeyaaga mashindano hayo kwa kufungwa goli 2-0 na wenyeji wa mashindano hayo Timu ya wilaya Makamba mkoa Burungu katika mashindano yanayofanyika kwenye uwanja wa Nkurunzinza Peace Park Complex ambapo timu ya Kibondo ilitolewa na Kombaini ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa kufungwa goli 1-0.

Uwanja wa michezo wa Nkurunzinza Peace Park Complex uliopo wilaya ya Makamba mkoa Burungu nchini Burundi ambapo mashindano ya ujirani mwema ya Lake Tanganyika Cup baina ya timu za mikoa ya Burundi na Kombaini za wilaya za mkoa Kigoma yanafanyika, Picha na Mwandishi wetu

Awali timu ya Kombaini ya Wilaya Buhigwe ya Tanzania ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuyaaga mashindano hayo baada ya kufungwa na timu ya Muyinga ya nchini Burundi baada ya kutandikwa mabao 2-1 ambapo hata hivyo na timu ya mkoa Muyinga ya nchini Burundi ilitolewa mashindano kwa kukiuka kanuni za mashindano.

Mjumbe wa kamati ya mashindano hayo Wilfred Lutera amethibitisha kuwa timu ya Muyinga ya nchini Burundi iliondolewa mashindano kwa kucheza Zaidi ya wachezaji 10 wenye umri wa Zaidi ya miaka 21 wakati kanuni inataka wachezaji wote wawe chini ya miaka 20 hivyo Buhigwe kupata nafasi ya kuendelea na mashindano.

Viongozi wa serikali ya Burundi na viongozi wa michezo Tanzania na Burundi wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Kombaini ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ambayo imefuzu kucheza nusu fainali ya mashindano ya ujirani mwema kwa kuitoa Kombaini wilaya ya Kibondo, Picha na Mwandishi wetu

Katika mchezo mwingine timu ya Kombaini ya Wilaya ya Nyanza ilitolewa kwenye mashindano hayo kwa kufungwa goli 2-1 na kombaini ya wilaya Ruyigi hivyo lufanya timu za Tanzania mbili na Burundi kuendelea na mashindano hayo ambapo Nusu fainali itafanyika siku ya jumatano.

Timu ya Kombaini ya Wilaya ya Makamba mkoa Burungu nchini Burundi ambayo imefuzu mashindano ya ujirani mwema kwa kuifunga kombaini ya Uvinza mkoani Kigoma kwa goli 2-0, Picha na Mwandishi wetu