Joy FM

Watendaji watakiwa kutumia mitandao ya kijamii kwa njia chanya

5 December 2025, 14:28

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Ibrahim Mwangarume, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imewataka watendaji wa Serikali za mitaa kutumia mitandao ya kijamii kwa manufaa ya maendeleo

Na Hagai Ruyagila

Maafisa Watendaji wa serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kutumia mitandao ya kijamii kwa manufaa ya maendeleo ya taifa na kuepuka kusambaza taarifa zinazoweza kuleta taharuki kwenye mitaa wanayoisimamia

Wito huo umetolewa na Kaimu mkuu wa Wilaya ya Kasulu Bw. Ibrahimu Mwangarume wakati akizungumza na baadhi ya maafisa watendaji wa serikali za mitaa wa halmashauri hiyo.

Amesema ni wajibu wa watumishi wa umma kuwa mabalozi wa wazuri wa matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuchochea maadili mema katika jamii.

Sauti ya Kaimu mkuu wa wilaya ya Kasulu Bw. Ibrahimu Mwangarume

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye amewataka watendaji hao kuendeleza uadilifu katika kazi zao ili kujijengea heshima na kuaminika zaidi mbele ya wananchi wanaowaongoza.

Sauti ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye

Naye mwenyekiti wa watendaji wa serikali za mitaa katika halmashauri ya Mji Kasulu Bw. Leonard Lugunguja amesema wataitumia mitandao ya kijamii kama fursa ya kujiongezea kipato na siyo kama chanzo migogoro au vurugu katika jamii.

Sauti ya mwenyekiti wa watendaji wa serikali za mitaa katika halmashauri ya Mji Kasulu Bw. Leonard Lugunguja
Mwenyekiti wa watendaji wa serikali za mitaa katika halmashauri ya Mji Kasulu Bw. Leonard Lugunguja, Picha na Hagai Ruyagila