Joy FM

Vijana waaswa kuwa wazalendo kwa jamii na Taifa

3 December 2025, 13:57

Mwenyekiti  Msaidizi Mstaafu  wa makanisa ya CPCT Mkoa wa Kigoma, Mchungaji Augustino Japhari Kizeba, Picha na Prisca Kizeba

Vijana  Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji  wameaswa kuacha kufanya   mambo yasiofaa katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti  Msaidizi Mstaafu  wa makanisa ya CPCT Mkoa wa Kigoma, Mchungaji Augustino Japhari Kizeba wakati wa kilele cha sherehe za vijana Kanisa la EAGT Mwasenga ambapo ameeleza vijana ni nguzo ya taifa na hawana budi kujitenga na mambo yasiyofaa bali wajikite katika kufanya kazi.

Sauti ya Mwenyekiti  Msaidizi Mstaafu  wa makanisa ya CPCT Mkoa wa Kigoma, Mchungaji Augustino Japhari Kizeba

Naye Mwenyekiti wa vijana Meshark Vasco amesema kuwa ameunda mikakati kwajili ya kuinua vijana kiuchumi na kiroho  ili kuondokana na hali ya  kuwa tegemezi.

Sauti ya Mwenyekiti wa vijana Meshark Vasco

Nao walezi wa vijana katika kanisa hilo John Goligosha Lamsoni na  Bi. Frola Yohana  wamesema kuwa  wazazi na walezi wanao wajibu wa kuwasaidia vijana ili waweze kufikia malengo  yao.

Sauti ya walezi

Baadhi ya vijana waliohudhuria sherehe hiyo wameeleza namna ya sherehe hiyo inavyolata umoja na mwitikio wa kukutanika kwa pamoja ili kuwa kitu kimoja.

Sauti ya baadhi ya vijana