Joy FM

Madiwani waazimia kuongeza ukusanyaji mapato Kigoma

2 December 2025, 12:39

Madiwani wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa katika mkutano wa kwanza baraza hilo, Picha na Lucas Hoha

Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia kwa madiwani wamazimia kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato kutoka shilingi milioni 400 hadi milioni 500 ili kusaidia kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi kwa wananchi

Na Lucas Hoha

Baraza la madiwani katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, limeadhimia kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka milioni 400 kwa mwezi hadi milioni 500 ili kuinusu Manispaa hiyo kutoka kwenye hatari ya kuondolewa hadhi ya kuwa Manispaa kutokana na ukusanyaji mdogo wa mapato.

Akizungumza kwenye kikao cha kwanza mara baada ya kuchaguliwa kuwa Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mussa Maulid amesema kipaumbele cha kwanza cha uongozi wake itakuwa ni kuongeza ukusanyaji wa mapato ili kuweka urahisi wa kutekeleza miradi ya maendeleo.

Aliyepo katikati ni Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Mussa Maulid akiwa katika kikao cha kwanza cha baraza la madiwani, Picha na Lucas Hoha

Naye Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Claiton Chipando mmarufi Baba Levo amesema katika suala la ukusanyaji wa mapato atashirikiana na Uongozi wa Manispaa ili kuhakikissha wanabuni vyanzo vipya vya mapato na fedha zitakazopatikana zitumike kwenye miradi ya maendeleo na kupunguza ushuru kwa wananchi.

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Claiton Chipando akizungumza kwenye baraza la madiwani, Picha na Lucas Hoha

Awali, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Kisena Mabuba pamoja na mambo mengine amesema kwa kushirikiana na madiwani anayo imani kuwa watawatumikia wananchi kwa uaminifu ili kutekeleza miradi inayogusa wananchi ikiwemo afya, maji na miundombinu ya barabara.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Kisena Mabuba, Picha na Lucas Hoha

Kabla ya kuanza kwa baraza hilo jipya la madiwani ambao wamechaguliwa na wananchi kwenye uchaguzi wameapa kiapo vha uaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania rasmi kuanza kuwatumikia wananchi.

Madiwani wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa katika mkutano wa kwanza baraza hilo, Picha na Lucas Hoha