Joy FM

Wazazi waaswa kufuatilia maendeleo ya watoto shuleni Kigoma

1 December 2025, 16:25

Wanafaunzi ambao wamehitimu wa elimu ya awali shule ya Cambridge Share, Picha na Prisca Kizeba

Wazazi wanapofuatilia maendeleo ya watoto wanaweza kugundua mapema kama mtoto ana matatizo ya kitaaluma, kitabia, au kihisia ili changamoto zikibainika, ni rahisi kupata suluhisho kabla hazijawa kubwa na ushiriki wa mzazi umethibitishwa kuwa na athari chanya kwenye matokeo ya mtoto shuleni, ikiwemo kujiamini, nidhamu, na uwezo wa kujitegemea.

Na Prisca Kizeba

Wazazi na Walenzi Manispaa ya Kigoma Ujiji, wameaswa kuendelea kuwasaidia watoto wao na  kufuatilia maendeleo yao shuleni.

Hayo yamesemwa na Mkurugernzi wa shirika la joy in the harvest Mwenge Munyombi wakati wa sherehe ya mahafali ya tatu ya watoto wa shule ya awali  Kembridge Share na kuwa wazazi wanao wajibu wa kufuatilia maendeleo ya mtoto wake ili kufahamu mienendo yake.

Sauti ya Mkurugernzi wa shirika la Joy In the Harvest Mwenge Munyombi
Mkurugenzi wa Joy In The Harvest akitoa cheti kwa mmoja wa wahitimu hao, Picha na Prisca Kizeba

Naye  Mkurugenzi Msaidizi wa shule hiyo Bi. Betha Silvest Bugaga ameleza namna wanaovyo wajibika katika  kumlinda mtoto dhidi ya ukatili anapokuwa katika mazingira ya shule.

Sauti ya Mkurugenzi Msaidizi wa shule hiyo Bi. Betha Silvest Bugaga

Mratibu Mkuu wa kituo cha shule ya awali Bi Magreth Pataleo Mushi ameeleza mbinu wanazozitumia katika kuwapa elim bora.

Sauti ya Mratibu Mkuu wa kituo cha shule ya awali Bi Magreth Pataleo Mushi

Nao baadhi ya wazazi wameipongeza shule hiyo kwakuwa na walim Bora na mahari katika kuwafundisha watoto wao

Sauti ya baadhi ya wazazi