Joy FM

Wazazi waaswa kuzingatia elimu ya awali kwa watoto

25 November 2025, 11:00

Mkurugenzi wa Shule ya Platonic day care Mwalimu Elirehema Simon akiwa kwenye picha na wanafunzi wahitimu wa shule hiyo, Picha na Sofia Cosmas

Wito umetolewa kwa wazazi na walezi wilayani Kigoma mkoani Kigoma kuwekeza kwenye elimu kwa kuhakikisha wanawasomesha watoto wao ili waweze kufikia ndoto zao.

Na Sofia Cosmas

Wazazi na walezi wametakiwa kuwapeleka watoto kusoma elimu ya awali  katika shule  zilizopo  karibu na makazi yao ili kuepusha usumbufu wa  watoto  kutembea umbali mrefu kwenda shule.

Wito huo umetolewa na Mwalimu Method Pastory Kokoye kwa niaba ya Mkurugenzi wa shule ya msingi na awali ya Ndameze wakati wa mahafali ya pili katika  shule ya awali ya PLATONIC DAY CARE iliyopo eneo la Kazegunga.

Amesema elimu ya awali ndio msingi mkubwa kwa watoto na hivyo wazazi hawana budi ya kuhakikisha watoto wanapata  elimu ya awali.

Sauti ya Mwakilishi wa Mkurugenzi Ndameze Mwalimu Method Pastory Kokoye
Wanafunzi waliohitimu elimu ya awali wakiwa kwenye Picha na uongozi wa shule na mgeni rasmi baada ya mahafali, Picha na Sofia Cosmas

Awali katika risala ya shule hiyo iliyosomwa na Mwalimu Belishada Masamaki ameeleza moja ya mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kukamilika kwa usajili kituo hicho  ambacho kwa sasa kitaitwa PLATONIC BLILIANT ACADEMY.

Sauti ya Mwalimu Belishada Masamaki

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shule ya Platonic day care Mwalimu Elirehema Simon amewaomba wazazi na walezi kuweka imani yao kwenye kituo hicho kwani ni kituo kinachotoa malezi bora kwa watoto.

Sauti ya Mkurugenzi wa Shule ya Platonic day care Mwalimu Elirehema Simon

Nao baadhi ya wazazi wa wahitimu wamepongeza juhudi za walimu wa kituo hicho kwa kuwapa watoto malezi bora.

Sauti ya baadhi ya wazazi wa wahitimu

Shule ya Platonic day care ilianzishwa 18  Februari  2024 kikiwa na watoto 5 mpaka sasa kina watoto 70 na watoto walio hitimu ni watoto 20 .