Joy FM

Wakristo waaswa kufanya kazi na kuacha utegemezi

24 November 2025, 14:34

Askofu  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Emmanuel Bwata, Picha na Prisca Kizeba

Wakristo wameaswa kufanya kazi kwa bidii na kuacha utegemezi

Na Prisca Kizeba

Waumi wa Dini ya Kikristo Katika Manispa ya Kigoma Ujiji wameaswa kufanya kazi ili waweze kuepukana na utegemezi na kujiletea maendeleo yao binafsi na kanisa kwa ujumla.

Hayo yameelezwa na Askofu  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Emmanuel Bwata wakati wa ufunguzi wa kanisi  Mtakatifu Yohana Anglikani lililopo Bagwe ambapo ameomba waumini kucha kuwa tegememezi na wajikite katika kfanya kazi.

Sauti ya Askofu  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Emmanuel Bwata

Aidha Askofu Bwata amekemea  baadhi ya viongozi wanotumia madalaka yao vibaya.

Sauti ya Askofu  Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Emmanuel Bwata

Naye Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana kanda ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Andasoni Bilasa amesema kuwa kila mshiriki anao wajibu wa kujibidisha katika kufanya kazi ili kuleta maendeleo ya kanisa.

Sauti ya Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana kanda ya Manispaa ya Kigoma Ujiji Andasoni Bilasa

Naye Mchungaji Nadhanael Amoni wa Kanisa hilo ameeleza namna waumini walivyojikita kupambana katika kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo liliogharim takribani shilingi milioni mia moja na arobaini na sita za kitanzania.

Sauti ya Mchungaji Nadhanael Amoni
Askofu wa Kanisa la Anglikana Emmanuel Bwataakiwa na wachungaji na waumini, Picha na Prisca Kizeba

Baadhi ya waumini wamesema kuwa katika kutimiza mlengo ya ujenzi wakanisa kumekuwa na changamoto mbalimbali licha ya kuwa limekamilika.

Sauti ya baadhi ya waumini