Joy FM

ENABEL yatoa msaada wa vifaa vya kufundishia Kigoma

20 November 2025, 15:43

Mkuu wa Mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro akiwa kwenye picha na viongozi mbalimbali wa elimu na wawakilishi wa Enabel, Picha na Lucas Hoha

Serikali ya Mkoa wa Kigoma imesema inaendelea kuthamini mchango wa mashirika mbalimbali yanayounga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu

Na Lucas Hoha

Shirika la Maendeleo la Ubelgiji ENABEL limekabidhi vifaa vya kidijitali vya kufundishia shuleni kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma ikiwemo komputa na sola vyenye thamani ya zaidi shilingi milioni 81 ili kuwepo na mazingira rafiki ya kujifunzia.

Elimu ni msingi wa maendeleo ya jamii na uchumi wa taifa lolote  na ili mfumo wa elimu uwe bora na wenye tija, unahitaji uwekezaji mkubwa katika rasilimali watu, miundombinu, na teknolojia.

Mkuu wa Mkoa Kigoma akipokea vifaa kutoka Enabel, Picha na Lucas Hoha

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma BaloziĀ  Simon Sirro ambaye anaeleza vifaa hivyo vitasaidia Mkoa kutekeleza malengo ya serikali ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Amesem kuna kila sababu za dhati kwa wakurugenzi wa Halmashauri kuvitunza vifaa hivyo ili visaidie kuzalisha wataalamu watakaokuwa na uwezo wa kushindana kwenye soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma BaloziĀ  Simon Sirro

Naye Katibu tawala wa Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema uwepo wa mashirika mbalimbali katika mkoa wa Kigoma yanayosaidia katika upande wa elimu imesaidia wanafunzi kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa hasa katika masomo ya sayansi.

Sauti ya Katibu tawala wa Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa
Mtaalamu wa Elimu ya Kidijitali kutoka Enabel Bi. Lotte Van Preat akizungumza, Picha na Lucas Hoha

Awali akikabidhi vifaa hivyo, Mtaalamu wa Elimu ya Kidijitali kutoka Enabel Bi. Lotte Van Preat amesema shirika hilo limekuwa likishirikiana na serikali katika masuala mbalimbali kupitia mradi wa wezesha binti lengo likiwa ni kuongeza uwezo wa walimu na wafunzi katika sekta ya elimu.

Sauti ya Mtaalamu wa Elimu ya Kidijitali kutoka Enabel Bi. Lotte Van Preat

Katika nchi nyingi zinazoendelea, serikali pekee haiwezi kukidhi mahitaji  na  ndipo mashirika ya maendeleo huingia na kutoa mchango mkubwa unaolenga kuinua viwango vya elimu na kuhakikisha upatikanaji wa elimu kwa wote