Joy FM

Vijana walia na vitendo vya ukatili Kigoma

18 November 2025, 13:04

Baadhi ya vijana wakiwa katika kongamano la Burudani lililoandaliwa kwa ajili ya utoaji wa elimu ya ukatili, Picha na Sadick Kibwana

Vitendo vya ukatili kwa vijana ni tabia au matendo yanayowadhuru kimwili, kihisia, kijinsia, au kijamii na ukatili huu unaweza kufanywa na watu wazima, wenzao, au hata mamlaka.

Na Sadick Kibwana

Vijana katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wameiomba Serikali kuendelea kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto ili vitendo hivyo viweze kupungua nchini.

Baadhi ya vijana wakiwa katika kongamano la Burudani lililoandaliwa kwa ajili ya utoaji wa elimu ya ukatili, Picha na Sadick Kibwana

Wakizungumza na kituo hiki katika tamasha la burudani na elimu lililofanyika eneo la taasisi ya Kigoma Vijana Development Alliance KIVIDEA, Vijana hao wamesema kwa sasa ni muhimu elimu kutolewa zaidi kuliko kuweka nguvu katika ukamataji wa waharifu.

Sauti ya vijana Manispaa ya Kigoma

Mwakilishi wa Vijana katika tamasha hilo kutoka shirika la KIVIDEA Leilah Yusuf ameleza umuhimu wa tamasha hilo kwa vijana kwa elimu waliyopata.

Sauti ya Mwakilishi wa Vijana katika tamasha hilo kutoka shirika la KIVIDEA
Baadhi ya vijana wakiwa wameshika mabango yanayoonyesha meseji ya kupinga ukatili wa kijinsia, Picha na Sadick Kibwana

Kwa upande wake, Mratibu kutoka KIVIDEA Nurdin Amani amesema umuhimu wa  tamasha hilo ni kufikisha elimu kwa vijana ili waweze kutambua namna ya kukabiliana na vitendo hivyo.

Sauti ya Mratibu kutoka KIVIDEA Nurdin Amani

Ikiwa ni wiki ya kuchukua hatua ambayo inafanyika kila mwaka mwezi novemba, Shirika la Kigoma Vijana Development Alliance KIVIDEA chini ya mradi wa Afya yangu Maendeleo yangu limefanya tamasha la elimu kuhusu ukatili wa kijinsia kwa kuhusisha makundi mbalimbali ya vijana.