Joy FM

Wananachi Kigoma waaswa kuzingatia lishe bora

17 November 2025, 13:20

Afisa lishe Mkoa wa Kigoma James Mbalabo akizungumza na Radio Joy FM kupitia kipindi cha Goodmorning Kigoma

Na Timotheo Leonard

Wananachi Mkoani Kigoma wameaswa kuzingatia lishe bora ya  makundi sita ya vyakula ili kuimarisha afya zao kwa  kuongeza virutubishi mwilini vinavyoimarisha  mwili na akili.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa lishe Mkoa wa Kigoma James Mbalabo wakati akizungumza na Radio Joy fm kupitia kipindi cha Goodmorning Kigoma  , na kusema  lishe ni muhimu kwa afya ya mwanadamu.

Afisa lishe Mkoa wa Kigoma James Mbalabo

Amesema mara nyingi magonjwa yasiyo ambukiza hutokea kutokana na na mtindo usiofaa wa vyakula na kwamba ni vyema kuzingatia matumizi sahihi ya vyakula kuepuka magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo moyo na kisukari.

Afisa lishe Mkoa wa Kigoma James Mbalabo