Joy FM

Waratibu wa JZK watakiwa kuleta matokeo chanya kwenye elimu

6 November 2025, 13:56

Washiriki wa jumuiya za  kujifunza katika mafunzo yanayofadhiliwa na mradi wa shule bora, Picha na Emmanuel Kamangu

Serikali imeendelea kuwanoa waratibu wa Jumuiya za Kujifunza ili waweze kusiamamia maadili ya kazi

Na Emmanuel Kamangu

Waratibu wa Jumuiya za Kujifunza (JZK) katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wametakiwa kuacha tabia ya kutanguliza posho mbele hasa wanaposhiriki mafunzo badala yake wazingatie maudhui yanayofundishwa ili kuleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Wito huo umetolewa na Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Bi Elestina Chanafi, wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa wasimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji ambapo amebainisha kuwa mafunzo hayo yatasaidia washiriki kuwajengea uwezo wa kutengeneza dira na kusimamia maadili ya kazi, jambo litakaloboreshwa zaidi ubora wa ufundishaji na ujifunzaji katika shule za msingi.

Sauti ya Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Bi Elestina Chanafi

Kwa upande wake, Mwezeshaji wa Mafunzo Bw, Jacob Chaudo, amesisitiza umuhimu wa kufanya maamuzi yanayotegemea takwimu kuliko hisia ili kubaini tatizo la kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi wa kike na upimaji wa mwenendo wa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Sauti ya Mwezeshaji wa Mafunzo Bw, Jacob Chaudo
Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Bi Elestina Chanafi, Picha na Emmanuel Kamangu

Afisa Elimu taluma Msingi Bw. Joseph Maiga, amesema anamatumaini washiriki watatumia ujuzi huo kuwajengea uwezo walimu wengine katika maeneo yao ya kazi ili kufanikisha azima ya kuwa na ufaulu mzuri kwa wanafunzi. 

Sauti ya Afisa Elimu Taluma Msingi Bw. Joseph Maiga

 Mafunzo haya yanayofadhiliwa na mradi wa shule bora yamehusisha wadau mbali mbali wa elimu wakiwemo wakuu wa shule na yamepangwa kufanyika kwa takribani siku nne ili kutoa fursa kwa washiriki kupata ujuzi wa kutosha juu ya namna ya kukuza taaluma shuleni.