Joy FM

Wananchi watakiwa kudumisha usafi wa mazingira Kasulu

27 October 2025, 12:42

Kaimu Katibu tawala wilaya KasuluIbrahim Mwangarume, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imeendelea kuhamasisha wananchi kuzingatia suala usafi wa mazingira kama ambavyo sheria ya mazingira ya 2016 inavyoelekeza kila mwananchi kuhakikisha mazingira yanayomzunguka yanakuwa safi salama

Na Hagai Ruyagila

Wananchi katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kuhakikisha wanadumisha usafi wa mazingira katika maeneo yao ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko ikiwemo ugonjwa wa Kipindupindu.

Wito huo umetolewa na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu, Bw Ibrahimu Mwangarume wakati wa maadhimisho ya usafi wa mazingira yaliyofanyika katika soko kuu la Kumsenga Halmashauri ya Mji Kasulu.

Bw. Mwangarume amesema kuwa usafi wa mazingira ni jambo la msingi katika maisha ya mwanadamu, hivyo ni wajibu wa kila mfanyabiashara na mkazi kuhakikisha mazingira yanakuwa safi wakati wote.

Sauti ya Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Kasulu, Bw Ibrahimu Mwangarume
Mwakilishi wa Katibu tawala sambasamba na viongozi wa Halmashauriya Mji wa Kasulu na Halmashauri ya Wilaya Kasulu wakifanya usafi katika sokola Kumsenga, Picha na Hagai Ruyagila

Kwa upande wake, Afisa Afya Mazingira na Mkuu wa kitengo cha Usafi na udhibiti taka Halmashauri ya Mji Kasulu Bw. Msafiri Nkimbili amezungumzia sababu ya ushiriki mdogo wa wananchi katika siku ya usafi lakini amesema tayari Halmashauri imebaini mwarobaina wa changamoto hiyo.

Afisa Afya Mazingira na Mkuu wa kitengo cha Usafi na udhibiti taka Halmashauri ya Mji Kasulu Bw. Msafiri Nkimbili
Afisa afya Mazingira na Mkuu wa kitengo cha usafi na udhibiti taka Halmashauri ya Mji Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Afisa Mtendaji wa Kata ya Kumsenga Bi. Rozina Mengo amesema wamaeneo yao yameendelea kuwa safi kutokana na kutoa hamasa kwa wananchi kushiriki katika shughuli za usafi wa jamii ili kukuepuka magonjwa ya mlipuko.

Sauti ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Kumsenga Bi. Rozina Mengo

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Kasulu wamesema usafi wa mazingira ni wamuhimu kwa kila kaya lakini wamekuwa wakishindwa kushiriki zoezi hilo la usafi kutokana na kukosa hamasa na elimukutoka kwa viongozi wao.

Sauti za baadhi ya wananchi wa wilaya ya Kasulu