Joy FM

Wazee Kasulu wataka jamii itambue mchango wao

2 October 2025, 09:34

Wazee wa Halmashauri ya Mji Kasulu wakiwa katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imeahidi kuendelea kuboresha maisha ya wazee kwa kuwasaidia kupata matibabu na mahitaji mengine muhinu kama sehemu ya kuambua mchango wao katika jamii.

Na Hagai Ruyagila

Baadhi ya wazee katika Halmashauri ya Mji Kasulu wameiomba serikali kuwaangalia kwa jicho la huruma na kutambua mchango wao muhimu katika jamii hii ni kutokana na kutengwa na jamii pamoja na familia zao.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wazee akiwemo Bi. Agness Bitazi, Bi Tatu Saidi na Bw Iddi  Rugiga wakati wa maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika katika halmashauri ya Mji Kasulu.

Wazee hao wamezungumzia changamoto zinazowakabili kwa kusema  kuwa kundi kubwa la wazee linakabiliwa na changamoto za maisha magumu, ukosefu wa huduma za msingi kama vile dawa, malazi na chakula, pamoja na kutopata heshima wanayostahili kutoka kwa familia na jamii kwa ujumla.

Sauti ya baadhi ya wazee katika Halmashauri ya Mji Kasulu

Mganga Mkuu wa halmashauri ya Mji Kasulu Dkt. Peter Janga ametolea kwa ufafanuzi wazee wanaotakiwa kuhudumiwa na serikali kwa kupewa dawa na matibabu ya bure.

Sauti ya Mganga mkuu wa halmashauri ya Mji Kasulu Dkt. Peter Janga

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Sabinus Chaula amesema kuwa serikali kupitia halmashauri hiyo imekuwa ikiendelea kutambua mchango wa wazee na inaweka mikakati ya kuhakikisha wanapata huduma bora kwa kuzingatia mahitaji yao.

Sauti ya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Sabinus Shaula
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu, Sabinus Shaula, Picha na Hagai Ruyagila

Naye, Mkaguzi wa Jeshi la polisi wilaya ya Kasulu Afande Mbaraka Luwongo ametoa wito kwa jamii kuwatambua wazee kama nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa huku akisisitiza kuwa mchango wao haupaswi kusahaulika.

Sauti ya Mkaguzi wa Jeshi la polisi wilaya ya Kasulu Afande Mbaraka Luwongo

Maadhimosho ya siku ya wazee duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo Oktoba Mosi, ikiwa ni fursa ya kutambua na kuheshimu mchango wa wazee katika jamii na taifa kwa ujumla.