Joy FM

Zitto kutenga bilioni 1 mikopo isiyo na riba Kigoma

18 September 2025, 15:30

Wananchi wa kata ya Kagera Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa katika mkutano wa kampeni wa chama ACT Wazalendo, Picha na Mwandishi wetu

Wananchi wa Kata ya Kagera Manispa ya Kigoma Ujiji, wameomba mgombea ubunge wa jimbola Kigoma mjini Zitto Kabwe kuwasiadia kutatua changamoto ya uwepo mikopo umiza.

Na Mwandishi wetu

Mgombea ubunge jimbo la Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameahidi kukomesha mikopo yenye riba kubwa maarufu kausha damu kwa wananchi endapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo, kwa kuanzisha mfuko maalum ambao ataweka shilingi bilioni 1 ili wananchi waweze kukopa bila riba. 

Zitto amesema hayo wakati wa kampeni zake za kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini zilizofanyika katika kata ya Kagera Manispaa ya Kigoma Ujiji, Septemba 17, 2025.

Mgombea ubunge jimbo la Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, Picha na Mwandishi wetu

Amesema wananchi wamekuwa wakishindwa kuendelea kutokana na mikopo umiza hali inayosababisha washinde kuendelea kimaisha.

Sauti ya Mgombea ubunge jimbo la Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe