Joy FM

Miradi 56 ya shilingi 64.7b kupitiwa na mwenge Kigoma

16 September 2025, 09:56

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa akiwa askari Polisi wakati wa kukimbiza mwenge Mkoani Kigoma, Picha na mwandishi wetu

Mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2025 zimeanza rasmi mkoani Kigoma ambapo miradi 16 ikitarajiwa kuwekewa mawe ya Msingi, mmoja kufunguliwa, 27 kuzinduliwa huku mingine 12 ikitembelewa na kukaguliwa.

Na Tryphone Odace

Mwenge wa uhuru umeanza mbio zake Mkoani Kigoma ambapo utapitia miradi 56  yenye thamani ya shilingi Bilioni 64.7 ambapo ukiwa mkoani humo mwenge huo wa uhuru utatembea kilimotea 777.1 katika halmashauri nane za mkoa Kigoma.

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Balozi Simon Sirro amesema hayo wakati akipokea mwenge wa uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa Kagera Fatuma Mwassa katika makabidhiano yaliyofanyika katika kijiji cha Nyakibuye Wilaya Kakonko Mkoani Kigoma.

Balozi Sirrtio alisema kuwa katika miradi itakayopitiwa na mwenge miradi 16 itawekewa mawe ya msingi, mmoja utafunguliwa, miradi 27 kuzinduliwa na miradi 12 itatembelewa.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa katika miradi inayotembelea na mwenge Wananchi wamechangia kiasi cha shilingi  milioni 283, halmashauri shilingi bilioni 1.6, wahisani shiliingi Bilioni 53 na serikali kuu ni bilioni 6.6.

Mkuu wa Mkoa Kigoma akipokea mwenge wa uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Picha na Mwandishi wetu

Katika siku ya kwanza ya mbio zake mkoani Kigoka Mwenge wa uhuru ulikimbizwa katika wilaya ya Kakonko ambapo Mkuu wa wilaya hiyo Evance Malasa amesema kuwa ukiwa Wilayani humo mwenge huo wa uhuru utatembelea miradi saba yenye thamani ya shilingi bilioni 2.2 ukikimbizwa kwa umbali wa kilometa 135.