Joy FM

Sangoma arudisha matunguli kanisani na kuokoka Uvinza

8 September 2025, 14:43

Matunguli yakiwa yamekusanywa mbele ya waumini wa kanisa la AGGC na Mganga wa jadi kuamua kuokoka, Picha na Safia Cosmas

Wito umetolewa kwa waganga wa jadi kuacha kupiga ramli chonganishi kwenye jamii kwani zimekuwa zikileta uchonganishi kwa wananchi na kuchochea migogoro

Na Sofia Cosmas

Wakristo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma wametakiwa kuachana na imani za kishirikina na badala yake kumrudia Mungu kwani imani hiyo zimekuwa zikichochea migogoro kwenye jamii.

Hayo yameelezwa na Mchungaji wa kanisa  la AGGCI Malagarasi lililop Wilayani Uvinza  Mch Meshack John  ambapo amewataka waamini wa dini ya kikristo na wasio wakristo kuachana na imani za kishirikina kwani imani hizo hupelekea athari kwa wananchi kama upotevu wa nguvu kazi kwa taifa.

Sauti ya Mchungaji wa kanisa  la AGGCI Malagarasi lililop Wilayani Uvinza  Mch Meshack John 

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha malagarasi akiwakilishwa na Acley Wiliamu amempongeza Mchungaji wa kanisa hilo kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuombea jamii na kuokoa maisha ya watu katika kijiji hicho.

Sauti ya Mwenyekiti wa kijiji cha malagarasi akiwakilishwa na Acley Wiliamu

Baadhi ya waumini akiwemo   Hashimu Ally ambaye alikua ni moja ya waganga wa kienyeji ambao walikua wanajihusisha na imani za kishirikina wamewashauri watu kuachana imani hizo na kumrudia Mungu kwani hakuna faida katika imani hizo mbali na uchonganishi kwa jamii.

Sauti ya Baadhi ya waumini akiwemo   Hashimu Ally