Joy FM

Wachakataji mazao ya uvuvi ziwa Tanganyika walia na masoko

1 September 2025, 15:27

Wavuvi wakiwa katika mtumbwi wakati wakivua samaki ziwa tanganyika, Picha na Mtandao

Serikali imesema itaendelea kuwasaidia wavuvi na wachakataji wa mazao ya uvuvi na kuwapatia masoko.

Na Kadislaus Ezekie

Wananchi  mkoani Kigoma ambao wamejikita katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba kwa kufuga samaki aina ya sato wa Ziwa Tanganyika pamoja na wachakataji wa mazao hayo, wameiomba serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwatafutia masoko makubwa ya ndani na nje ya nchi, baada ya kuongeza uzalishaji wa samaki hao.

‎Mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba, umekuwa na tija kwa wafugaji ikiwa ni matokeo chanya baada ya serikali kuwawezesha vizimba hivyo kwa mkopo nafuu matokeo makubwa yakionekana kwa kuzalisha mazao mengi.

Wateja walionao ni wa ndani, soko ambalo halikidhi wingi wa mazao wanayopata kutoka katika vizimba wakati wa uvunaji wakiwa tayari wamevuna  awamu ya kwanza.

Sauti ya wavuvi na wachakati wa mazao ya uvuvi

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ikiwa katika ziara ya kukagua miradi ya serikali katika sekta hiyo, inaahidi kutafuta soko la uhakika sambamba na wawekezaji kuombwa kuja kuwekeza katika mradi huu.

Sauti ya mwakilishi wa Wizara ya uvuvi na kilimo