Joy FM

Wafanyabiashara 4026 wasajiliwa Kigoma

29 August 2025, 17:30

Mkuu wa Wilaya Kigoma Dr. Rashid Chuachua akiwa katika kongamano la SHIUMA, Picha na Orida Sayon

Wafanyabiashara wadogowadogo Mkoani Kigoma wametakiwa wametakiwa kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa na taasisi za benki na Halmashauri ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Na Orida Sayon

Shirikisho  la umoja wa machinga Tanzania (SHIUMA) kanda ya magharibi limefanya kongamano la kumpongeza Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa uboreshaji wa miundombinu ya biashara.

Kongamano hilo limefinyika leo katika uwanja wa katubuka sekondari  manispaa ya kigoma ujiji ikihusisha mikoa ya  Katavi, Kigoma,Tabora na Rukwa

Akitoa taarifa ya hali ya usajili wa wafanyabiashara ndogondogo, Afisa biashara  Baraka Fubusa amesema jumla ya wafanyabiashara 4026 wamesajiliwa katika mfumo wa wanyabiashara ndogondogo mkoani Kigoma.

Sauti ya Afisa biashara  Baraka Fubusa
Ni maandamano ya wafanyabiashara wakielekea katika kongamano la SHIUMA, Picha na Orida Sayon

Aidha ameeleza kuwa wafanyabiashara wengi wamekuwa na madeni  mengi  katika taasisi za kifedha, na kukosa mwitikio wa kulipia vitambulisho vya wafanya biashara ndogondogo hali inayopelekea kukosa mikopo ili kujikwamua katika biashara zao.

 Licha ya uwepo wa mafanikio na uboreshwaji wa miundombinu ya biashara ukosefu wa elimu ya mikopo na kukosa mitaja ni miongoni mwa changamoto zinazowakumba wafanyabiashara.

Sauti ya wafanyabishara

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt Rashid Chuachua akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma katika kongamano hilo amewataka wafanyabiashara hao kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa na taasisi za kifedha na mikopo inayotolewa na halmashauri ili kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt Rashid Chuachua
Mkuu wa Wilaya Kigoma akipika wakati alipotembelea monyesho ya mama lishe kwenye kongamano la SHIUMA