Joy FM

Wahitimu darasa la saba waaswa kuwa na maadili mema

25 August 2025, 14:08

Wahitimu wa darasa la saba Cambrige Shire Academy, Picha na Sofia Cosmas

Wito umetolewa kwa shule binafsi kuanza kufuata mabadiliko ya mtaala mpya ambao umetolewa na serikali ili kuboresha sekta ya elimu nchini.

Na Sofia Cosmas

Watumishi wa umma na sekta binasi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wametakiwa kuondoa utengano na chuki badala yake washikamane  kuleta wazo la pamoja   katika kuijenga Kigoma na  Taifa la Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Cambrige Shire Josephati Chales Njige  wakati wa mahafari ya nne ya darasa la saba katika shule ya msingi na awali ya Cambrige Shire Academy ambapo amewataka watumishi wa Umma na Sekta binafsi kushirikiana kwa pamoja ili kuijenga Kigoma na taifa kwa ujumla.

Sauti ya Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Cambrige Shire Josephati Chales Njige 

Awali katika risala kwa mgeni rasmi iliyosomwa na Meneja wa shule hiyo ya Cambrige Shire Academy Mwl Lazaro Kiguja amesema mafanikio ya shule hiyo yanatokana na misingi na malengo waliyojiwekea kama anavyoeleza hapa.

Sauti ya Meneja wa shule hiyo ya Cambrige Shire Academy Mwl Lazaro Kiguja

Akijibu risala mgeni rasmi katika sherehe hizo, Afisa kutoka Ofisi ya Udhibiti Ubora  Rusi Nyanda  amewapongeza walimu wa Shule hiyo na kuahidi kubeba changamoto walizoziainisha kuzipeleka panapohusika.

Sauti ya Afisa kutoka Ofisi ya Udhibiti Ubora  Rusi Nyanda 

Kwa upande wao, baadhi ya wazazi na wanafunzi katika shule hiyo wamewataka wazazi na walezi kuwafundisha watoto wao hasa mtaala mpya kwa vitendo.

Sauti ya baadhi ya wazazi na wanafunzi katika shule hiyo