Joy FM

Mabaraza ya watoto yasaidia kupungua ukatili Buhigwe

13 August 2025, 15:29

Watalamu wa idara ya maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Buhigwe wakiwa na mkaguzi wa Polisi Miyonga ambaye ni mkuu wa dawati la jinsia na watoto.

Wito umetolewa kwa wazazi na walezi kuendelea kutoa taarifa na ushirikiano pindi matukio ya ukatili yanapotokea ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa.

Na Emmanuel Kamangu

Mabaraza ya watoto Wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma yametajwa kuwa chachu ya kupungua kwa  matukio ya ukatili kwa watoto.

Amebainisha hayo Afisa maendeleo ya jamii wilayani Buhigwe Bw, Christopha kajange katika kikao ambacho kimewahusisha viongozi wa Dini na baadhi ya wananchi ikiwa ni kutoa tathimini ya hali ya ukatili wilayani humo ambapo amesema kwa kasuhirikiana na shirika la kuhudumia watoto Dunia  UNICEF wameendelea kujizatiti  kuhakikisha mtoto anabaki salama zidi ya vitendo vya ukatili.

Sauti ya Afisa maendeleo ya jamii Wilayani Buhigwe Bw. Christopha Kajange
Afisa maendeleo ya jamii wilayani Buhigwe, Picha na Emmanuel Kamangu

Kwa upande wake, Afisa ustawi wa jamii wilayani humo Bw. Agrey  Mwambete amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanakuwa karibu na watoto ili kujua kila jambo wanalolipitia wakiwa nje na nyumbani.

Sauti ya Afisa ustawi wa jamii wilayani humo Bw, Agrey  Mwambete

Baadhi ya viongozi wa dini wilayani  humo wamesema wataendelea kushirikiana na serikali ili kuhakikisha jamii inaondokana na vitendo vya ukatili.

Sauti ya baadhi ya viongozi wa dini Wilayani  Buhigwe

Aidha Mkuu wa dawati la jinsia na watoto wilayani Buhigwe mhadhamu miyonga amewataka wazazi na walezi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi pindi wanapoona matukio ya ukatili na kuepuka kuyashugulikia kifamilia.  

Sauti ya Mkuu wa dawati la jinsia na watoto Wilayani Buhigwe Mhadhamu Miyonga