Joy FM

Waziri Gwajima ataka elimu ya ufundi iwe chachu ya fursa kwa vijana

30 July 2025, 11:57

Waziri  wa maendeleo ya jamii, wanawake, jinsia na makundi maalumu Mh. Doroth Gwajimaakiwa na wahitimu wa veta Kigoma

Vijana waliohitimu mafunzo katika chuo cha veta Kigoma wametakiwa kutumia ujuzi walioupata kuchangamkia fursa zilizopo kujiajiri.

Na Orida Sayon

Waziri  wa maendeleo ya jamii, wanawake, jinsia na makundi maalumu Mh. Doroth Gwajima ameelekeza wakurugenzi wa maendeleo ya jamii nchini kupeleka wadau maendeleo katika vyuo vya ufundi stadi veta kutoa elimu ya fursa kwa wanafunzi.

Waziri Doroth Gwajima ametoa maagizo hayo wakati wa ziara iliyofanyika katika chuo cha ufundi stadi veta kigoma iliyolenga kuwatunuku vyeti wahitimu wa kozi za muda mfupi na kutembelea ofisi ya dawati la jinsia VETA Kigoma ikiwa ni moja ya utekelezaji wa mradi wa wezesha binti unaofadhiliwa na shirika la Enabel.

Sati ya Waziri  wa maendeleo ya jamii, wanawake, jinsia na makundi maalumu Mh. Doroth Gwajima

Aidha waziri Gwajima amewataka vijana kutumia ujuzi waliopata kama chanzo cha kujipatia ajira na kuajiri kwa manufaa yao familia huku wakipinga kila aina ya ukatili na matumizi ya dawa za kulevya.

Sati ya Waziri  wa maendeleo ya jamii, wanawake, jinsia na makundi maalumu Mh. Doroth Gwajima

Mkurugenzi Mkazi wa enabel nchini Tanzania Bw. Koenraad Geonkint amesema Kiasi cha shilingi billion 3 za kitanzania zimewekezwa kusaidia programa ya mafunzo ya ufundi katika vyuo vya ufundi stadi ili kuwezesha vijanaa zaidi ya 2300 kupata mafunzo ya ujuzi Mkoani Kigoma.

Sauti ya Mkurugenzi Mkazi wa enabel nchini Tanzania Bw. Koenraad Geonkint

Baadhi ya wahitimu waliotunukiwa vyeti vya kozi za muda mfupi akiwemo Asha Omary Mohammed wanaeleza namna ujuzi utakavyowanufaisha.

Sauti ya Baadhi ya wahitimu waliotunukiwa vyeti vya kozi za muda mfupi