Joy FM

Wasafiri waombwa kutoa taarifa za uvinjifu wa amani

23 July 2025, 16:05

Mrakibu wa Polisi DTO Patrick Damas ni Mkuu wa usalama barabarani wilayani Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Wasafiri wametakiwa kutoa taarifa za uvunjifu wa amani wakati wakiwa safarini.

Na Hagai Ruyagila

Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama barabarani Wilayani Kasulu limetoa wito kwa wasafiri wote wanaotoka Wilaya hiyo kuelekea maeneo mengine kutoa taarifa mapema wanapobaini dalili zozote zinazoashiria uvunjifu wa amani au hatari yoyote inayoweza kuhatarisha usalama wao wakiwa safarini.

Wito huo umetolewa na Mrakibu wa Polisi DTO Patrick Damas ni mkuu wa usalama barabarani Wilayani Kasulu wakati akitoa elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari ofisini kwake.

Sauti ya Mrakibu wa Polisi DTO Patrick Damas

Aidha DTO Afande Damas amewashauri wananchi kuhakikisha wanakuwa na mawasailiano ya moja kwa moja na askari ili kurahisisha utoaji wa taarifa pindi hali ya dharura au tukio la kihalifu linapotokea.

Sauti ya Mrakibu wa Polisi DTO Patrick Damas

Baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Kasulu wamesema kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi watakapoona au kuhisi vitendo vya uvunjifu wa amani vinatokea wawapo safarini au sehemu yoyote ni vizuri maana itasaidia hatua ziweze kuchukuliwa kwa haraka.

Sauti ya baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Kasulu