Joy FM

Wananchi wapewa elimu kujikinga na majanga ya moto Kigoma

9 July 2025, 09:51

Maaskari wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoani Kigoma wakiwa katika soko la Kigoma Mjini wakitoa elimu ya kujikinga na majanga ya moto, Picha na Hamis Ntelekwa

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Kigma limewataka wananchi kuendelea kuchukua hatua za kukabiliana na majanga ya moto ambayo yanaweza kujitokeza katika maeneo yao.

Na Esperance Ramadhan

Baadhi ya Wananchi Mkoani Kigoma wamepatiwa elimu ya kuzima moto pindi linapotokea tatizo la moto na  kuhakikisha wanachukua tahadhari ilikunusuru majanga yanayoweza kujitokeza ikiwemo vifo .

Akizungumza na wananchi wa kata ya Kigoma mjini Manispaa ya Kigoma Ujiji Mrakibu Msaidizi Michael Maganga ambaye pia ni kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Kigoma amesema elimu waliyoitoa ya kuzima moto ni mbunu za kujiokoa waowenyewe pindi tukio la moto linapotokea.

Sauti ya Mrakibu Msaidizi Michael Maganga ambaye pia ni kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Kigoma
Gari la Jeshi la zimamoto na uokoaji likiingia katika soko la Kigoma Mjini wakati wa zoezi la utayari wa kukabiliana na majanga ya moto, Picha na Hamis Ntelekwa

Naye  Mkaguzi Bahati Salum ambaye pia ni Mkuu wa mkitengo cha usalama dhidi ya majanga ya moto Mkoani Kigoma amesema wataendelea kutoa eluimu kwa wananchi ili kuondoa hali ya taharuki pindi majanga ya moto inapotokea.

Sauti ya Mkuu wa mkitengo cha usalama dhidi ya majanga ya moto mkoani Kigoma

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wameeleza namna wanavyochukuwa tayari kukabiliana na majanga ya moto  hasa kwenye maeneo ya mkusanyiko.

Sauti ya baadhi ya wananchi