Joy FM

BoT yataka wakulimu kutohifadhi fedha ndani

2 July 2025, 16:01

Mkuonekano wa fedha za Tanzania, Picha na BoT

Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kuzingatia matumizi na utunzaji bora wa fedha.

Na Mwandishi wetu Uvinza

Wakulima Mkoani Kigoma wametakiwa kuachana na utamaduni wa kuhifadhi fedha ndani na badala yake kutumia huduma za kibenki ili kuondokana na adha ya upotevu wa fedha ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara.

Kaimu Meneja Msaidizi idara ya huduma jumuishi za fedha kutoka Benki kuu ya Tanzania BOT Edmund Mbokosi amesema kumekuwa na utamaduni wa baadhi ya wakulima hususani maeneo ya vijijini kuhifadhi fedha kwa kuzichimbia chini jambo ambalo si salama.

Sauti ya Kaimu Meneja Msaidizi idara ya huduma jumuishi za fedha kutoka BoT

Na hapa wakulima nao wanaeleza ni kwa namna gani uhifadhi wa fedha kwa njia ya kienyeji umekuwa ni mwiba kwao.

Sauti ya wakulima kutoka Wilayani Uvinza

Kwa upande wake, Mchumi kutoka Benki kuu ya Tanzani Lucas Magazi amesema wakulima wanatakiwa kuachana na mikopo umiza ambayo imekuwa ikiwarudisha nyuma kila kukicha.

Sauti ya Mchumi kutoka Benki kuu ya Tanzani Lucas Magazi

 Kwa pande wake, Afisa mtendaji kata ya Kalya Jeremaya Fanueli amesema  elimu waliyopatiwa itasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaondoa wananchi kwenye changamoto ya mikopo umiza.