Joy FM

BoT yapiga marufuku fedha za kigeni kutumika kufanya miamala nchini

21 May 2025, 14:37

Muonekano wa Benki Kuu wa Tanzania BoT, Picha na tovuti ya BoT

Ni kosa la kisheria kunukuu, kutangaza au kubainisha bei kwa kutumia fedha za kigeni, kulazimisha, kuwezesha au kupokea malipo kwa fedha za kigeni.

Na Glory Paschal

Benki kuu ya Tanzania BoT imesema malipo yote ya bidhaa na huduma yanapaswa kufanyika kwa kutumia shilingi ya Tanzania lengo ikiwa ni kuongeza thamani fedha ya ndani.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha BoT, Bw. Emmanuel Akaro, wakati akizungumza katika semina ya waandishi wa habari iliyofanyika katika ofisi za Benki Kuu jijini Dar es Salaam, kuhusu Kanuni za Matumizi ya Fedha za Kigeni za Mwaka 2025.

Sauti ya Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha BoT, Bw. Emmanuel Akaro

Amesema kwa mujibu wa Kanuni hizo, bei na malipo ya bidhaa na huduma zote ndani ya nchi yanapaswa kufanyika kwa Shilingi ya Tanzania.

Sauti ya Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha BoT, Bw. Emmanuel Akaro

Amesema  ni kosa la kisheria kunukuu, kutangaza au kubainisha bei kwa kutumia fedha za kigeni, kulazimisha, kuwezesha au kupokea malipo kwa fedha za kigeni, au kukataa malipo yanayofanyika kwa shilingi ya Tanzania.

Sauti Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha BoT, Bw. Emmanuel Akaro