Joy FM

Wakulima walia na bei ya pamba Kasulu

9 May 2025, 12:54

Baadhi ya Wakulima wa zao la pamba Wilayani Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima wa pamba ili waweze kulima pamba kwa wingi.

Na Hagai Ruyagila

Wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu, mkoani Kigoma, wameiomba serikali kuongeza bei ya ununuzi wa zao hilo ili wakulima waweze kuzalisha kwa wingi.

Katika taarifa ya maendeleo ya uzalishaji wa pamba ambayo imetolewa na viongozi wa AMCOS mbalimbali halmashauri ya wilaya ya Kasulu wamesema bei ya sasa ni ndogo na imesababisha baadhi ya wakulima kukata tamaa ya kuendelea na zao hilo la Biashara  na kulazimika kuhamia kwenye mazao mengine.

Efraimu Erasto katibu wa Buyonga Amcos ni miongoni mwa viongozi wa AMCOS wanaeleza baadhi ya changamoto zinazowakabili katika kilimo cha zao la pamba huku suala la Bei likitakiwa kutazamwa kwa jicho la tatu.

Sauti ya Wakulima wa zao la pamba wilayani Kasulu

Meneja wa Kampuni inajihusisha na ununuzi wa pamba katika Wilaya ya Kasulu ambayo ni Uvinza Ginnery, Bw. Mabula William, amesema kampuni hiyo ina uhitaji mkubwa wa zao hilo kutokana na mahitaji ya viwanda hivyo wameweka mikakati ya kuongeza bei ya zao hilo.

Mkaguzi wa Pamba wilaya ya Kasulu Michael Kihiga, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya Meneja wa Kampuni inajihusisha na ununuzi wa pamba

Akizungumzia kuhusu zao la pamba, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Isaac Mwakisu, amesema kwa kushirikiana na mnunuzi wa zao hilo wataangalia uwezekano wa kuongeza bei, kwa lengo la kuhakikisha wakulima wananufaika na zao la pamba.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Isaac Mwakisu
Mkuu wa Wilaya Kasulu Mkoani Kigoma Kanal Isaac Mwakisu, Picha na Hagai Ruyagila

Mkaguzi wa pamba wilaya ya Kasulu Michael Kihiga amesema uwepo wa maafisa ugani wa BBT umeweza kusajili kwenye mfumo wakulima 671wenye jumla ya Ekari 2977.16

Sauti ya Mkaguzi wa pamba wilaya ya Kasulu Michael Kihiga